Header Ads

ZITTO,KAFULILA NA WAZANDIKI WENZENU MMESHUSHUKA SHUUU!!



Na Happiness Katabazi
' GWIJI la muziki wa dansi Duniani, Koffi Olomide ' Mopao' , aliwahi kusema hivi hivi:'' Uongo unapanda lifti na ukweli unapanda ngazi'.

Koffi Olomide  alikuwa ana maanisha taarifa za uongo uwa tabia ya kusambaa haraka sana  na kwamba ukweli unachukua muda mrefu kufika yaani kujulikana  kwasababu ni kama mtu anayetumia lifti hufika haraka kule aendako na yule anayepanda ngazi kwa kutumia miguu uchelewa kufika kule aendako licha ni lazima atafika aendako .

Sisi watu wa Kabila la Wanyambo toka Wilaya ya Karagwe mkoani Kagera tuna msemo usemao  hivi; "Kabambone, " ahemuka omu mbaga. 
Kwa tafsiri ya lugha ya Kiswahili manaake ni ; ' Atakaye kutamba hadharani ,aibu zake huanikwa juani.'.


Nimelazimika kutumia nukuu hiyo ya Koffi kwasababu Mwaka Jana Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila, aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya PAC, Zitto Kabwe, Mbunge wa Njombe,Deo Filikunjombe na wabunge wengine wazushi walimzushia uongo aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Eliakim Maswi .

Kuwa ni wezi wameiba Fedha za Tegeta Escrow na kuwa  Fedha za Escrow ni Fedha za umma na kuwa viongozi hao wameziiba uzushi ambao uliaminiwa na watu wasiyopenda kufikiri na kufanya utafiti lakini watu wenye akili timamu na tunaopenda kufanya utafiti Kama Mimi niliipingana wazi wazi na Kamati ya Zitto na Kafulila na wale wote waliokuwa wakisema Fedha za Escrow ni mali za umma, na kwamba Muhongo na Maswi walioshiriki kuiba Fedha hizo na ushahidi Kuwa nilipinga uzushi na fitna zilizokuwa zimefanywa na wabunge ni makala mbalimbali .

 Desemba 23 Mwaka 2014 , Rais Jakaya Kikwete Katika mkutano wake na  wazee wa Dar es Salaam Katika hotuba yake alisema Fedha za Escrow Si mali ya umma na Kama siyo mali ya umma  hawezi  kuwashitaki kwa mashitka ya wizi wa fedha hizo Kama tulivyokuwa tumeaminishwa Ujinga na baadhi ya wabunge na Kamati ya Zitto na Kafulila Kuwa Fedha za Escrow ni mali ya umma na zimeibwa kwa Magunia watu waliotajwa kwenye ripoti ya PCA kwakutumia Benki ya Mkombozi mali ya Kanisa Katoliki.

Itakumbukwa pia Professa   Muhongo Katika hotuba yake wakati akijiuluzu  nafasi ya uwaziri wa Nishati na Madini alisema anajiuzulu   kwasababu ya fitna, majungu, Chuki za kisiasa na wafanyabiashara ila anaimani aliifanya Kazi yake kuitumikia taifa kwa uzalendo wa Hali ya juu na ipo siku ukweli utajulikana.Na ukweli imejulikana Juzi Kuwa waliozushiwa tuhuma zile na wanasiasa manyang'au.. Ni suala la muda tu, tuipe Mahakama nafasi ifanyekazi yake.


Baada ya Sakata la Escrow kushika kasi na wananchi Wengi wakajenga Chuki na viongozi hao na serikali kwa ujumla, Balozi Sefue alitangaza kumsimamisha Kazi Maswi ili kupisha uchunguzi, Muhongo na aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Fredrick Werema walijuzulu nafasi zao  huku wakiitwa ni mafisadi wa fedha za Escrow, Rais Jakaya Kikwete alimtimua Kazi aliyekuwa Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka na Mbunge William Ngeleja, Andrew Chenge walivuliwa madaraka yao katika CCM na kushitakiwa katika Sekretarieti ya Maadili ya Umma na hadi sasa bado chombo hicho hakijatoa uamuzi wake dhidi ya mashauri yao.

Baada ya viongozi Hao waliotuhumiwa Katika Sakata la Escrow kujiuzulu , Mtandao wa Watetezi  wa Haki za Binadamu unaunganisha asasi  za kiraia zinazotetea Haki za binadamu ( THIRD- Coalition), wakimpata Tuzo Kafulila na Kafulilia akasema hivi  " Naamini 'scandal'  ya Escrow itaiondoa CCM madarakani Kama Goldenburg ilivyoiondoa  KANUNI madarakani' alisema Kafulila.


Mei 8 Mwaka huu,  Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alitoa ripoti za uchunguzi kuhusu Maswi na Profesa Muhongo ambapo alisema baada ya Kamati ya Maadili ya Sekretarieti ya Umma kuwachunguza imebainika Maswi,Muhongo hawakuhusika Kutenda makosa ya jinai ,ukiukwaji wa Maadili Katika Sakata la Escrow hivyo hawana hatia.

Pia Sefue alitoa ripoti nyingine ya uchunguzi kuhusu Sakata la Operesheni  Tokomeza Ujangili ,Mawaziri wote waliojiuzulu kwa sakata hilo hawana hatia kwa kuwa waliwajibika kisiasa tu.Kisheria tunaita ( Ministerial Responsibility).


Mawaziri waliojiuzulu kutokana na Sakata la Tokomeza ni Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk.Emmanuel Nchimbi, aliyekuwa Waziri wa Maliasili, Balozi  Khamisi Kagasheki, aliyekuwa Waziri wa Kilimo na Chakula Dk.Mathayo David  na aliyekuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Vuai Nahodha.

Sakata la Tokomeza lilivaliwa njuga na mbunge James Lembeli na wenzake.

Kabla sijaenda Mbali ,napenda kutoa pongezi zangu za dhati kwa  Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue ( Baba Careen)  kwa kazi nzuri aliyoifanya yeye na timu yake ya uchunguzi ambayo ilichunguza tuhuma dhidi ya Muhongo na Maswi na mwisho wa siku juzi;

Balozi   Sefue alitoka  hadharani na kukata mzizi wa fitna na kutoa ripoti ya uchunguzi wa sakata la Escrow ambapo alisema timu yake ya uchunguzi imebaini Muhongo, Maswi hawana hatia ya jinai wala ukiukwaji wa maadili ya utumishi wa umma .

 Umma uliaminishwa na wanaisiasa uchwara aina ya Zitto  na wazushi wenzake Kuwa maofisa hao wa serikali kuwa ni mafisadi wa Escrow na walinufaika na Fedha za Escrow na Fedha za Escrow na mali ya umma licha Muhongo alisema siyo Fedha za umma.

Sasa ni wazi tuhuma dhidi ya Muhongo na Maswi zilikuwa ni tuhuma   za kizushi na visasi vya kisiasa ,biashara na ambazo zilizushwa na wanasiasa uchwara yaani baadhi ya wabunge ambao walitumia Bunge letu kuendesha uzushi huo .

Hali iliyosababisha wananchi kuichukia serikali, CCM, na viongozi lakini hatimaye Juzi vyombo vya uchunguzi vya serikali vimewaona hawana hatia na ripoti hiyo ni wazi Kafulila, Zitto Kabwe na wazandiki wenzako mmeshushuka shuu.

 Gazeti la Tanzania Daima la Jumapili, Mei 18 mwaka 2014, lilichapisha makala yangu iliyokuwa na kichwa cha habari kisemacho ( KASHFA YA ESCROW  ISITUVURUGE).

Miongoni mwa haya za makala hiyo ni haya if upatapo hapa chini ; 
Tujifunze kutokana makosa, tusiwe wepesi kuamini   kila kitu kinachoibuliwa na baadhi ya wanasiasa wetu uchwara Kwani wengine ni Mavuvuzera wa wafanyabiashara, makampuni  na wanasiasa,na makuadi wa Makundi yanayoasimiana Katika magomvi Yao ama ya Kugombea Tenda Fulani, Biashara , urais Mwaka 2015  na kulipizana visasi vitendo ambavyo havina maslahi ya taifa zaidi ya kutaka kuvuruga umoja wetu.Tusiwape nafasi wahuni hawa.

Disemba  23 Mwaka 2014 nilichapisha makala yangu iliyokuwa na kichwa cha Habari kisemacho ; (   WALIOMUITA PRO.MUHONGO NI MUHONGO KAMA JINA LAKE AIBU YAO).

Miongoni mwa haya zilizokuwa Katika Katika makala hii ni hizi hapa ; 

WALE wazushi,Visarata Mtaa,Washambenga,wenye nongwa Kama ndugu wa mume ambao Katika zogo la Escrow,walimu hukumu Waziri wa Nishati na Madini, Professa Sospiter Muhongo Kuwa ni Muhongo kama jina lake na kwamba ni fisadi wa Escrwo Leo hii wameziweka wapi sura zao? 


Licha ya Profesa Muhongo kutoa utetezi wake kupitia hotuba yake ndani Bunge ambapo pamoja na mambo mengine ,msomi Huyo alisema Fedha za Escrwo siyo za umma watu wakiwemo wanasiasa uchwara ambao ni wabunge walimpinga na kumuhukumu Kuwa ni Muongo mkubwa Kama jina lake na kwamba Fedha za a Escrow ni za umma. 

Lakini Jana Baba mwenye nyumba nyumba, Profesa Jakaya Kikwete katika hotuba yake alikubaliana na Muhongo Kuwa Fedha zile siyo za umma ni za IPTL na hazijaibwa wala Kubebwa kwa Magunia Kama Zitto Kabwe wakati akisoma ripoti ya PAC bungeni alisema Fedha za Escrow zilibebwa kwa Magunia bila kufuata Taratibu ya Sheria ya Benki Kuu. 

Waswahili wanamsemo wao usemao ' Mnafki hafi hadi ameumbuka'. Hivyo wanafki,Majaji mama DDP ,DCI ,majaji ,Mashushushu wa 'Kichina' ,mabush Lawyer ,wazushi na mahakimu uchwara ambao mlijipachika majukumu yasiyo ya kwenu ya kuhukumu Watu na kuwaita wakina Muhongo ni wezi ,wamekula Rushwa ,wamechota Fedha ya umma ya Escrow hotuba ya jana imewaumbua. 

Naendelea kusisitiza tuache tabia ya kuhukumu au kushabikia jambo wakati Hatuna vielelezo Vya kutosha Kwani tukae tukijua uzushi unaumuiza watu wasiyo na hatia Katika baadhi ya mambo machafu wasiyo yatenda. 

Leo hii kila kona watu wamepandikizwa chuki Mbaya sana ambapo baadhi ya wananchi ambao wao wakisikia jambo hawataki kilifanya utafiti wanaliamini, wanaamini Muhongo ni fisadi, kaiba Fedha za Escrow Kumbe ni uzushi tu unafanywa na wahuni wachache kwa Malengo Yao binafsi. 

PAC ilipotosha umma Katika ripoti yake ilisema Kiwango Cha Fedha kilichokuwa kwenye Akaunti ya Escrow ni Sh.Bilioni 306.7. Wakati ukweli ni kwamba kiasi kilichokuwa kwenye Akaunti ya Escrow ni Bilioni 202.9. PAC ilisema Fedha za Escrow ni za umma, Rais amewaumbua amesema siyo za umma ni za IPTL. 

Mnaolazimisha kuwa fedha za Escrow ni za umma endeleeni kulazimisha, ila haitawasaidia maana tayari mjadala huo Baba mwenye nyumba yaani Rais Kikwete aliufunga mjadala huyo kwa kusema fedha za Escrow siyo za ummma. 

Waliomuita Profesa Muhongo ni Muhongo Kama jina lake kwasababu eti alisema Fedha za Escrow Si za umma, ni dhahiri shahiri hotuba ya jana imewaumbua. Mabingwa wa fitna kajipageni upya ili tukianza Mwaka mmoja 2015 muibuke na jungu jingine mAana shughuli kubwa mnayoifahamu ni kuwazushia wenzenu uongo. 

Binafsi naamini ipo siku ushauri wa kisheria uliotolewa na aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali,Jaji Werema utakuja kueleweka ,ni suala la muda. Mungu ibariki Tanzania. 

Disemba 12 Mwaka 2014 niliandika Makala yangu iliyokuwa na kichwa cha Habari kisemacho ; (KIKWETE USIWASIKILIZE  'BUSH LAWYER' KATIKA ESCROW).

Baadhi ya haya zilizomo Katika makala hii nikimfuata zao; 

Sakata la Escrow  pamoja nalo limeibua au kuwezesha mambo mengi sana. Limekuwa kama mtego wa panya ambao waliokuwemo na wasiokuwemo wote wanaingia na baadhi ya watu wakauchukulia huu mwanya kutimiza  haja na matakwa yao ya kisiasa. 

Januari 24 Mwaka 2015, niliandika makala kupitia ukurasa wangu wa Facebook na Blogg yangu ya www.katabazihappy.blogspot.com. ,iliyokuwa na kichwa cha Habari kisemacho ; (MUNGU AKULINDE  SOSPETER MUHONGO )

Baadhi ya haya za Makala hii ni hizi hapa ;

LEO  saa tano asubuhi,Januari 24 Mwaka 2015 , aliyekuwa  Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo alitangaza rasmi kujiuzulu nafasi hiyo ya uwaziri kwasababu ya zogo  la Escrow.

Tangu mwanzo kupitia makala yangu msimamo wangu niliweka wazi Kuwa naunga mkono Utendaji kazi wa Profesa Muhongo na hata Leo hii ninavyoandika makala hii sitabadilisha msimamo wangu Kuwa Kwangu Profesa Muhongo ni Miongoni mwa Mawaziri wa Nishati na Madini ambao nimewashuhudia Kuwa ni mawaziri ambao wameacha alama ya kukumbukwa.

Pia tangu mwanzo nilisema wazi kupitia makala zangu mbalimbali kwa jicho la Sheria Katika zogo la Escrow Hakuna Mashitaka ya wizi Kama baadhi ya watu walivyokuwa wakiwa hukumu Moja kwa Moja watu  waliotajwa kwenye zogo la Escrow Kuwa ni wezi na kwamba Fedha za Escrow zimeibwa.

Waswahili wanasema penye ukweli, uongo ujitenga. Hivyo ipo siku ukweli wa hili zogo la Escrow utakuja kujulikana nani muhasisi wake?  Kwanini waliliasisi zogo hili?,Muhongo alishiriki kwa kiasi gani Katika jambo Hilo?Ni kweli Katika Utawala wa Muhongo Wizara ya Nishati ilipata Hasara na kwamba Hakuna jambo lolote la maendeleo alilolifanya?

Nchi hii Ilipofika hivi sasa, majungu, fitna,ushirikina, uzandiki Ndio umetawala na umeshika hatamu.Watu wasiyo na hatia na siyo kwenye Nyanja za siasa tu wanaangamia kwa ushenzi huo.

Imekuwa nchi ya watu tunaopenda Ujinga Ujinga na uzushi halafu na mbaya zaidi tabia hizo zinafaywa na wanaume amba wanawake nyumbani eti tunajiaminisha nchi hii itapata maendeleo kwa haraka.

Hivyo Muhongo muachie Mungu, yeye ndiyo muweza wa yote, endelea kulitumikia taifa Lako kwa uaminifu ila kwa taadhari pia  Kwani Tulipofika sasa watendaji waaminifu na wachapakazi nchi hii HIvi sasa nikama hawatakiwi.


Narudia tena wale wote mabingwa wa kufanya binadamu wenzao kwa Lengo tu la kupata maslahi Fulani ikiwemo biashara, vyeo Mkae mkijua ipo siku Mungu atawaadhibu.

Kumbukeni hawa mnao wafanyakazi ufedhuli nao wana Mungu na Mungu wao wala siyo kipofu wala kiwete anayetembelea Magongo.Ipo siku Mtalipwa Ubaya mnaofanyia  wenzenu.Aminini  hivyo.

Mungu akutangulie Muhongo nenda kafanyekazi na wasomi wenzio achana na hawa wanaume 'wachambue Michele'  ambao wametawaliwa na husuda na fitna na unafki na vichwa vyao wanavitumia kwaajili ya Kufugia nywele badala ya kufikiri.

Pia niliandika na makala nyingine nyingi tu za Kusema Katika Sakata la Escrow kuna uzushi mwingi tuwe makini na nilichokiambulia kutoka kwa baadhi ya watu wenye akili za kipuuzi ni matusi ,vitisho na kuambiwa Mimi ni Kimada wa Profesa Muhongo wakati Si kweli.

Mungu si Athuman wala Juma, Ripoti za Balozi Sefue kuhusu Escrow zimethibitisha pasipo shaka  kuwa watuhumiwa wale yaani Muhongo, Maswi waliokuwa wakitajwa kwenye kashfa ya Escrow hawana hatia.

Sijui wale wanasiasa waliotuaminisha uongo ambao ulipandikiza chuki za wazi na taharuki katika jamii dhidi ya wananchi na Maswi na Muhongo sijui wanajisikiaje hivi sasa maana ni kama watu waliojisaidia bila kujitawaza.

Na wanasiasa ambao wengi wanajinsia ya kiume ambao ndiyo walikuwa wazushi wakubwa na vizabinazabina ,washambenga na wazushi walikuwa  wakiongozwa na Kafulila, Zitto,Filikunjombe, Ole Sendeka na wengine.

Itakumbukwa Sakata la Escrow lilivyopamba Moto wabunge Hao na wengine walikuwa ni watu wenye Mithili waliopandwa na Pepo mchafu wa kuwazushia watu uongo.

Bila haya wabunge Hao vijana kiumri waliuaminisha umma Kuwa Maswi, Muhongo ni mafisadi wa Escrow huku mioyoni mwao wakijua siyo kweli ila kwasababu roho wa kishetani alikuwa amewavaa alikuwa akiwatuma kuwashuhudia wenzao uongo mzito Kama ule kwasababu wanazozijua wao.

Lakini kuna Msemo usemao Mnafki hafi hadi ameumbuka. Sasa Zitto na wajumbe wake wa Kamati ya PAC, Kafulilia na wazushi wenzao bado wapo hadi hivyo siku hadi siku wanazidi Kuumbuka kwa unafki na uzandiki wao walioufanya Katika Escrow.

Aliyekuwa wa kwanza kuwaumbua ni Rais Kikwete Katika hotuba yake kwa wazee wa mkoa wa Dar es Salaam, ya Disemba 23 Mwaka 2014  ambapo pamoja mambo mengine Kikwete aliwaambu wazandiki hao Kuwa Fedha za Escrow siyo mali za umma, na Fedha za Escrow hazijaibwa Kama ilivyokuwa ikidaiwa na ' mashushushu wa Kichina' yaani Kamati ya PAC iliyokuwa ikiongozwa na Zitto.

Wa pili kuwaumbua mabingwa hao wa uzushi   ni Balozi Sefue , ambaye kupitia ripoti ya Sefue aliyoitoa kwa waandishi wa Habari kuhusu uchunguzi wa Sakata la Escrow ni kwamba uchunguzi umebaini Maswi, Professa Muhongo hawana hatia ya jinai wala Maadili kinyume na ilivyodaiwa na Kamati ya Bunge ya Bunge ya PAC iliyokuwa ikiongozwa na Zitto Kuwa walihusika na wana makosa ya jinai na walinufaika na Fedha za Escrow. 

Baada ya Balozi Sefue kutoa ripoti yake ,Kafulila Jana alinukuliwa  na Gazeti la Mtanzania akisema hivi ; " Uamuzi wa Ikulu  kumsafisha Maswi na Muhongo ulitarajiwa kwa Sababu ninao ushahidi  wa barua  unaonyesha  Ikulu kuhusika  Katika Sakata  hili  na Ndio  Sababu  Rais  Kuvuta miguu".

Wakati Kafulila akitaka Kuanza kuaminisha umma Ujinga wake huo wa kupinga vitu visivyopingika anasahau Ikulu hiyo hiyo iliruhurusu Mnikulu , Shabani Gurumo , Mbunge wa Jimbo la Sengerema,William Ngeleja , Andrew Chenge, Professa Tibaijuka  kushitakiwa Katika Sekretarieti ya Maadili na mashauri Yao yanaendelea.

Kafulila tulia unyolewe nywele Kwani hivi sasa wewe na wazushi wenzake Katika Escrow ni zamu yenu kuumbuliwa na ukumbuke Kuwa bado ile Kesi ya Madai ya kashfa ya Sh.  Bilioni 310 iliyofunguliwa na Kampuni ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL)  kwa kushirikiana na kampuni ya Pan African Power Solutions (T) Limited na Mwenyekiti Mtendaji   wa kampuni hizo, Harbinder Sigh Seth imemfungilia Kafulila kesi hiyo ya madai ya kashfa.


Katika kesi hiyo, walalamikaji kwa pamoja wanaiomba mahakama imwamuru Kafulila   awalipe fidia ya Sh.Bilioni 310   kwa madai ya kutoa kashfa dhidi yao kwa kuwatuhumu kujipatia fedha kutoka katika Akaunti ya Escrow, kwa njia zisizo halali na Kesi hiyo inaendelea na ipo siku itafikia Tamati kwa kufahamu Kafulila alisema kweli au aliizushia uongo kampuni hizo Kama alivyowazushia wakina Maswi na Muhongo.Tuvute subira.

Itakumbukwa Kuwa ni Kafulila huyu huyu kipindi kile alipozusha Sakata la Escrow ,Waziri Mkuu Mizengo Pinda alisema amesikia taarifa zake hizo kuhusu Escrow na Pinda akamwagiza Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) afanye uchunguzi wake Kama Fedha za serikali Katika Sakata Hilo la Escrow ziliibwa au zilitumika vibaya au hizo Fedha zilikuwa ni za umma.

Lakini Pinda baada ya kutoa agizo hilo kwa CAG  ,Kafulila huyu huyu aliibuka na kumdhalilisha Pinda Kuwa anataka kuficha ukweli kuhusu Escrow na anataka kuwalinda mafisadi wa Escrow  Hali iliyosababisha watu wenye akili timamu nikiwemo Mimi kuandika makala ya kumshambulia Kafulila na kumuonyesha ni jinsi gani asivyoheshimu Utawala wa Sheria na Kanuni,kwani Kafulila yeye Katika Escrow alikuwa ni Mtoa taarifa tu lakini ghafla akawaka kujitwika majukumu mengine ya Ujaji,upelelezi majukumu ambayo siyo yake.

Na siku Muhongo alipojiuzulu,Maswi aliposimamishwa Kazi,Tibaijuka alipofukuzwa Kazi na rais , huyu huyu Kafulila, Zitto na wenzake waliitokeza hadharani na kujisifia Kuwa wao ni wanasiasa wanaipenda  nchi Yao Kwani wamefanikisha kuibua tuhuma za ufisadi na kushikilia Bango hadi vigogo hao wakaondoshwa madarakani na Kafulila akapewa  Tuzo na akachekelea sana.

Juzi Balozi Sefue katoa ripoti ya uchunguzi wa Sakata la Escrow dhidi ya Muhongo na Maswi na Kusema Kuwa  hawana hatia, eti Kafulila kafufuka sijui katokea makaburi gani  anasema alitarajia Ikulu ingewasafisha sasa najiuliza Ikulu sikuhizi ni Maji,sabuni au dodoki maana vifaa hivyo ndiyo vinamsafisha Mtu aendapo bafuni kuoga.

Uwenda Kafulila Ana wazimu siyo bure. Kama Kafulila alitarajia  Ikulu ingewasafisha viongozi hao ni kitu gani kilimuwasha Kipindi kile hadi akashupalia lile  Sakata la Escrow? 

Ni kitu gani kilikutuma  ukapokee ile Tuzo uliyopewa na wanaharakati wale na wakati akipokea ile Tuzo akachekelea sana na kujitapa yeye ni mwanaume wa Shoka Kwani skendo aliyoibua imeweza kuwaondoa madarakani viongozi hao wa serikali na kwamba Sakata Hilo la Escrow eti itaiangusha serikali na CCM.

Kwa ripoti ya Balozi Sefue , ni wazi kabisa Taasisi iliyompa tuzo  Kafulila nayo imeumbuka Kwani ilifanya papara Kumpa Tuzo hiyo bila kusubiri taarifa ya Matokeo ya uchunguzi wa kashfa hiyo ilitolewa.

 Hiyo Tuzo  bora ukaitupe jalalani maana haina maana tena kwasababu ripoti ya uchunguzi ambayo ilifanya uchunguzi kwa mujibu wa sheria kwani chombo kilichofanywa uchunguzi kipo kwa mujibu wa sheria, kimebaini tuhuma zilizoibuliwa na Kafulila ni uzushi na zimeshindwa kuishawishi Timu ya uchunguzi imkute na hatia Muhongo na Maswi.

Namshauri  Kafulila ,Zitto hivi sasa wafunge   Midomo Yao   na Wakubali  Kuwa sasa ni zamu yako ya kuumbuliwa kwa uzushi wao  na sisi waandishi wachokonozi na wananchi tusiyopenda  uzushi hatutakubali tena kuendelea kuwavumilia kusikiliza uzushi wenu ambao umeligharimu taifa na kuwathiri watu wasiyo na hatia tutawaanika adharani na kuwashushua.

Tumechoka na vitendo Vya kizushi vinavyofanywa na wanasiasa wa aina yako ambao Inadaiwa Kabla ya Kuzusha Sakata fulani mnahongwa  kwanza Fedha na wafanyabiashara walionyimwa Tenda au Kuzuiwa mambo Yao na baadhi ya viongozi wa serikali wasiyotaka Rushwa na kuburuzwa na wafanyabiashara hao halafu nyie  baadhi ya wabunge uchwara mnamchukua ugomvi huo mnaingiza ndani ya Bunge na kuanza Kuzusha na kuchafua baadhi ya watendaji wa serikali na mawaziri na hii tabia ya kishenzi inayofanwa na wabunge washenzi washenzi imeota mizizi hapa nchini.

Na hotuba ya Rais Kikwete ya Disemba 23 Mwaka 2014, Ripoti ya uchunguzi ya Escrow iliyotolewa na Balozi Sefue hazina Ishara nzuri Katika hatima yako ya kushinda tena Kiti cha Ubunge Katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba Mwaka huu na pia siyo Ishara nzuri Katika ile Kesi ya Madai inayokukabili pale Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.

Na ile Kesi ya kumtolea lugha ya matusi Mkuu wa Wilaya Kule Kigoma bado inakukabili. Tatizo Lako Kafulila hujui madhara ya kushitakiwa ndiyo mAana unaamua Kujitoa fahamu kufanya vitendo Vya kihayawani vinavyosabisha kushitakiwa .

Nakutuma nenda kwa Mwenyekiti wa Chama cha TLP, Augustine Mrema, wakili Mabere Marando hata Tundu Lissu watakueleza madhara na Usumbufu,Kadhia waliyoipata wakati waliposhitakiwa Katika Kesi mbalimbali.

Lissu na umwamba wake aliposhinda Kesi ya kupinga Ubunge wake alilia Machozi nje ya Viwanja Vya Mahakama Kuu na kulaani waliokuwa wamemshitaki Kwani walikiwa wakimkera na kumsababishia Usumbufu.Sasa wewe bado unawashwa na ukae ukijua hizo Kesi zitakusumbua sana.

Kama ni watu wa Kupenda kujifunza basi Watanzania na wafadhili ambao ni mabingwa wa Kupenda kuhukumu watuhumiwa wa kashfa mbalimbali bila kusikiliza upande wa pili na kufanya utafiti mtakuwa mmejifunza sasa na kuacha kuamini harakahara tuhuma zinazoiburiwa na hawa wanasiasa wetu uchwara dhidi ya watendaji wa umma na wanasiasa wenzao.

Minilishajifunza  muda mrefu sana ndiyo maana hata katika  Sakata la escrow lilipoibuliwa nilitaadhalisha kwani  hawa wanasiasa Wengi wanatabia za uzushi sana na Chuki na kupitia ripoti ya Sefue, hotuba ya Kikwete ya Disemba 23 Mwaka 2014 .

Ripoti  ya uchunguzi kuhusu aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo  ambaye nae alisimamishwa Kazi na Katibu Mkuu Kiongozi kufuatia azimio la Bunge lilomuusisha na Madai ya kutoa Rushwa wa Bunge ili Bajeti ya Wizara ipite lakini mwisho wa siku Katibu Mkuu Kiongozi baada ya Timu yake kufanya uchunguzi ikamuona Jairo Hana hatia.

Pia azimio la Bunge Mwaka 2008 lilivyoona eti kulikuwa na Rushwa Katika mkataba wa Richmond na hivyo kufanya aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa kujiuzulu na mawaziri wengine wa Nishati na Madini Nazir  Karamagi,  Msabaha kujiuzulu.

Lakini Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa inayoongozwa na Dk.Edward Hosea ilifanya uchunguzi kuhusu azimio Hilo la Bunge kuhusu mkataba wa Richmond na kubaini Hakuna Rushwa yoyote na wabunge hao akiwemo Waziri wa sasa Dk.Harrison Mwakyembe walishiriki kikamilifu kuipata matope TAKUKURU Kuwa inakumbatia mafisadi. Dhambi sana.

Waandishi wa Habari wenzangu wote wale waliokuwa wakitumiwa au kutumika vibaya kuchafua watu Katika Sakata la Escrow Ndio ripoti ya Balozi Sefue, hotuba ya Kikwete iwafunze na muache kutumiwa kuchafua watu wasiyonahatia maana hakuna ubishi kuwa baadhi ya vyombo vya habari vilitumika kikamilifu kuchafua Muhongo,Maswi katika sakata la Escrow na kulikuza jambo hilo.

Wosia wangu wa Zitto,Kafulila na wabunge wengine acheni tabia ya kujifanya Nyie ndiyo wabunge vijana mnaopenda kujitanguliza mstari wa Mbele Kudai mnakashfa dhidi ya wanasiasa wenzenu halafu mna wachafua wee na kuwaletea madhara hadi wanaamua kujiuzulu nyadhifa zao na wengine kusimamishwa Kazi na wengine kusababisha kupotea Katika ulingo wa siasa uzushi wenu.

Siwakatazi msiibue machafu ila Kabla ya kuyaibua akikisheni mnafanya hivyo mkiwa na nia safi  siyo nia ovu. Katika Sakata hili la Escrow tangu mwanzo ushahidi wa mazingira na mlituhumiwa wazi wazi Kuwa mlikuwa mkitumika vibaya Kuwaumiza kwa Niaba Mbaya Muhongo, Maswi kwasababu eti Maswi na Muhongo waliwataka kuendeshwa na mfanyabiashara mmoja  ambaye mfanyabiashara Huyo alikuwa akiwatuma ila baadhi ya wabunge,wanasiasa wengine na vyombo Vya Habari kuwapaka matope Muhongo,Maswi na serikali kwa ujumla Kuwa serikali ni ya kifisadi na haijali wafanyabiashara wazawa. 

Na Spika Anne Makinda baada ya Kamati ya PAC siku ile kumaliza kusoma mapendekezo yake ,mama huyo alisema hivi ' Nyie baadhi ya wabunge acheni kuwazushia wenzenu uongo na kwamba siku mtakapokamatwa na kuweka Rumande sitamsaidia Mtu maana kuna wengine mnatumiwa na wafanyabiashara huko nje magomvi yao mnayaamishia ndani ya bunge'. 

Taifa linalokuwa na aina ya wabunge wa aina hii ambao ni wazushi, Wapika majungu dhidi ya mawaziri wetu na watendaji wa serikali ni hatari sana.

Ndiyo maana siku zote Nawapongeza wale wote walitangulia Mbele za Haki ambao walioanzisha kitu SHERIA na UCHUNGUZI.

Hakuna ubishi Katika Sakata la Escrow Kama Wanasheria na wachunguzi ambao ni wanataaluma ya Sheria na wachunguzi wasinge shirikishwa kufanyakazi zao za kitaaluma Katika Sakata hili ni wazi Muhongo na Maswi Wangezidi kuzikwa wakiwa hai na wanasiasa hawa wenye hulka za mapakashume ambao haya taaluma ya uchunguzi na Sheria hawana  kwa uzushi na Chuki tu ambazo Hazina tija kwa taifa letu.

Mbunge mzima tena mwanaume yaani Zitto, Kafulila Mishipa ya fahamu ilikuwa ikiwasimama kuwazushia uongo Muhongo na Maswi huku wakijua ni uongo, ni hatari ya Mungu na ndiyo maana wanasiasa wamekuwa anaaminiki kwa Yale wanayoyasema kutokana na baadhi ya wanasiasa wenzao Kama hawa ambao wanazushia wenzao uongo na kuwaletea madhara makubwa kisaikolojia,kuwashushia heshima Katika Jamii na sehemu wanaofanya kazi .


Hivi mlifikiri ukweli hautokuja kujulikana? Na kwa Kuwa Zitto na Kafulila hamnaga aibu sidhani hata kama mmeshtushwa na ripoti hiyo ya Balozi Sefue ya kuwaona hawana hatia Maswi na Muhongo.

Na bado Mungu ataendelea kutumia watu wake hapa hapa Duniani kuwadhibu hasa wewe Zitto maana Tayari Mungu alilitumia  Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kukuadhibu Kuitupilia Mbali Kesi yako dhidi ya Chadema ambayo ulikuwa umeomba Mahakama hiyo itoe amri ya Kuzuia vikao Vya Chadema visikujadili.

Pia Mungu akatumia watu wake hapa hapa Duniani yaani Mwanasheria wa Chadema,Tindu Lissu na uongozi wa Chadema, kukutimua uanachama na ulivyotimuliwa uanachama ukajiuzulu nafasi ya Mwenyekiti wa PAC na ukajiuzulu nafasi ya Ubunge.

Ukaenda kuanzisha Chama cha ACT  ,kitendo ambacho sio Moja ya vipaumbele Vya Watanzania na ukajinasibu eti ipo siku utashika nafasi ya juu ya uongozi Katika taifa hili.

Watanzania tumeishakubaini tabia yako hivyo hatuitaji Kuwa na kiongozi mwenye tabia za kizushi kushika madaraka ya juu ya taifa hili maana atakitumbukiza taifa mtoni.

Yote hayo yanayokukuta ni malipo ya Mungu maana Mabaya uliyowatendea wenzako Hao ,wenzako walilia na Mungu wao na Mungu ndiyo anawalipia kwa kasi  na Ikulu ndiyo imeisha msafisha Maswi, Muhongo Kuwa hawana hatia lakini wewe hadi Leo Hakuna aliyetengua uamuzi wa kufukuzwa Kwao na Chadema unahesabika Kuwa ni Mwanachama aliyefukuzwa na Chadema kwa tabia chafu na kuvunja Katiba ya Chadema na tuhuma Usaliti.

Lakini wale wakina Muhongo, Maswi na wengine wao hawajafukuzwa vyama vyao, na wameonekana hawana hatia hivyo Zitto umeumbuka Kwani ulilolikusudia kwa watu hawa halijakuwa na bado utazidi Kuumbuka na kuchapwa bakora ya Mungu hadi utakapoungama dhambi hiyo maana watu Wengi sana walilia na kusikitika nakumshitakia Mungu ,Kwa uzushi mlimzushia Profesa Muhongo na Maswi ambao walikuwa wakichapakazi vizuri Katika Wizara ya Nishati na Madini.

Kilichokuwa kikiniuma Katika Sakata la Escrow Kuwa kuna watu Kama Maswi, Muhongo wanaangamizwa bila hatia kwasababu nilikuwa nafahamu fika kuna mchezo mchafu ndani ya Sakata Hilo na Mlengwa mkubwa alikuwa ni Muhongo na Maswi ambao wakikataa kuburuzwa na 'Bwana'  wa wanasiasa ambao machakubimbi .

Ni huyu huyu Zitto ,Kafulila na wanasiasa uchwara wenzao Mara kwa Mara wamekuwa wakilalama majukwaani na Kwenye vyombo Vya Habari Kuwa serikali inatumia Fedha za umma  vibaya   Kumbe wakati mwingine uzushi 
Wanaouzushaga Ndiyo  unasababisha serikali itumie Fedha kuunda Timu za uchunguzi kuchunguza ukweli    wa tuhuma za uzushi unaoanzishwagwa  na wanasiasa hao uchwara mahiri wa Kuzusha uongo Katika baadhi ya mambo wanayoyazusha Kwenye Escrow.

Hivi Zitto,Kafulila na wenzako uwa mtapataga  raha gani tena  mnavyo shiriki  kuangamiza wenzenu kwa kuwashuhudia uongo ili wafukuzwe kazi na kufikishwa Mahakamani ,kitendo ambacho ni wazi Zitto,Kafulila hamumuogopi  Mungu kabisa maana moja ya amri ya Mungu inakataza binadamu usimshuhudie mwenzio uongo.

Na pia Mungu alituagiza binadamu wote tu pendane.Lakini Kwa kitendo hiki cha uzushi  wewe Zitto ,Kafulila na wazushi wenzako katika  Escrow ambapo mlimzushia  uongo Muhongo na Maswi ni wazi mmepuuza   agizo la Mungu lilotutaka  kila mmoja ampende jirani yake Kama a navyopenda nafsi yake . 

Kama kweli mnatekeleza agizo Hilo la Mungu la Mpende jirani yako Kama unavyoipenda nafsi yako ,Zitto na PAC na wazushi wengine msingediriki kushupaza shingo kuwashuhudia uongo wakina Muhongo na Maswi Kama mlivyo wafanyia unyama ule.

Sasa hata Kama maagizo hayo ya Mungu na amri yake hiyo ya usimshuhudie mwenzio   uongo lakini mkapuuza amri hiyo ya Mungu  ,ni wazi Nyie ni watu anakuogopwa sana na sisi watu wa Mungu maana Kama mmediriki kupuuza maagizo ya Mungu aliyewaamba ndiyo mtaacha kupuuza maagizo yanayotolewa na binadamu wenzenu ?

Mngekuwa na upendo wa kweli kwa Muhongo,Maswi msingediriki kuwatendea ule unyama na ukatiri mliowatendea wa kuwazushia uongo mtakatifu Kama ule uliosababisha Muhongo, Maswi kuchukiwa na umma na kunuka bila hatia na kuachia nyadhifa zao.

Mara kwa mara kupitia mitandao ya kijamii nimekuwa nikisema dhambi aliyotendewa Muhongo,Maswi Katika Escrow itamtafuna Zitto na genge lake liloungana kutunga uzushi ule ambao uliwaletea madhara makubwa Maswi na Muhongo lakini kwakuwa ni majasiri na walikikabidhi jambo hili kwa Mungu na walijua hawana kosa walilotenda walikaa kimya na kuacha vyombo husika vifanye kazi yake na mwisho wa siku ukweli utabainika na kweli ukweli imebainika Kuwa Zitto na wazushi wenzake wakiwashushia uongozi kwa Sababu wanazozijua.Mtakuja kulaaniwa.

Sisi watu wa Kabila la Wanyambo toka Wilaya ya Karagwe mkoani Kagera tuna msemo unasema   hivi;    "Kabambone, " ahemuka omu mbaga. 

Kwa tafsiri ya lugha ya Kiswahili manayake  ni ; ' Atakaye kutamba hadharani ,aibu zake huanikwa juani.'

Sasa Msemo huu unatufandisha  kwamba Zitto na wazandiki wenzake waliozusha Sakata la Escrow dhidi ya Profesa Muhongo na Maswi  awali wakati wakizusha Sakata Hilo walitamba sana hadharani lakini sasa aibu zao zimeanikwa juani na ripoti ya uchunguzi wa Balozi Sefue imeachwa uchi mchana kweupe Kamati ya PAC iliyokuwa ikiongozwa na Zitto, Filikunjombe  na muhasisi wa uzushi wa Escrow Kafulila na wazandiki wengine. 

Uwa najiuliza hivi Zitto,Kafulila na wazushi wenzake walinyonya kweli maziwa ya mama zao Miezi Tisa?Au walinyweshwa uji wa Muhogo badala ya kunyonya maziwa ya  Mama zao  ndio maana  wanatabia hizi  za uzushi uzushi?

Wakati mwingine uwa najiuliza ya wanaume hawa wazushi sijui wa naishije na wake zao majumbani?

Aipendezi kabisa mwanaume tena Ana ndevu anavaa suruali na Kufunga Mkanda kiunoni kusifika kuwa na tabia za kizandiki kama hizi za kizushi na kuwashuhudia binadamu  wenzenu uongo na  mzushi kwa maslahi yenu binafsi.

Nasielewi  hawa wanasiasa wazushi wa Escrow wanaishi vipi na wake zao majumbani  Maana mwanaume kuwa  na tabia chafu Kama hii ya uzushi tena kuzushia uongo watu waliowazidi  umri Kama Professa Muhongo,Maswi ni wazi hawa wanasiasa vijana wana matatizo   makubwa na wasiyo acha hiyo tabia ya uzushi watalaaniwa.

Biblia inatuambia Kuwa Shetani ni Baba wa uongo, hivyo wale wote walimzushia uongo Profesa Muhongo, Maswi  kuwa walipata mgao wa fedha za Escrow wakati ni uongo baba Yao ni shetani na wao ni mashetani maana Mtoto wa Mungu azungumzi wala kumshuhudia jirani yake uongo lakini Ituo,Kafulila na wazandiki wenzao waliwashuhudia majirani zao yaani (Maswi,Muhongo uongo) .

 Naviomba  vyombo ya dola vimsake Kafulila awapatie huo ushahidi wa hiyo Nyaraka anayodai ni ya Ikulu  inayoonyesha Ikulu  ilikuwa imepanga kuwasafisha Muhongo na Maswi ili Ikulu ione hiyo barua kweli ni ya Ikulu?Ilitoka Ikulu kwenda kwa Kafulila kwa kufuata utaratibu?

Na Kama hiyo barua anayodai ni ya Ikulu na ikaja kubainika siyo ya Ikulu haraka sana Huyo afikishwe mahakamani kwa kosa la kutoa taarifa za uongo kwa umma maana serikali ikiendelea kumlea Mzushi huyu ataendelea na tabia yake chafu ya kulala na kuamka na Kuzusha mambo mazito ambayo yanaligharimu Maisha watu ikiwa ni kuaribia Maisha,hadhi zao, kuliingiza taifa Katika matatizo makubwa ikiwemo  kunyimwa misaada na wafadhili .


Professa Muhongo,Maswi kwakuwa Nyie ni wa kristo ,ni watu wazima na mnaakili timamu mlitangulia kuliona jua najua mliumizwa  sana na uzushi wa Zitto na wazandiki wenzake nawashauri wasameheni kabisa,msilipe kisasi Kwani jukumu la kulipa kisasi ni la Mungu na  ZABURI ya 35 katika Biblia inasema wazi jukumu la kulipa kisasi ni la Mungu Mwenyewe siyo binadamu na ripoti ya Balozi Sefue, Hotuba ya Kikwete ya Disemba 23 Mwaka Jana, niwazi Mungu ameishatumia ZABURI ya 35 kupigana nao wote waliokuwa wakipingana nanyi.

Niitimishe Kwa kunukuu nukuu ya Koffi Olomide " Uongo Una panda lifti ,ukweli Una panda ngazi'. 

Na ni kweli ,ukweli  katika Sakata la Escrow ulipoanda ngazi ukachelewa kufika ,wasiyo na hatia wakasurubiwa kwa uzushi lakini hatimaye Juzi ukweli ule wa escrow uliokuwa unakuja taratibu kwa kupanda   ngazi ulifika ulikokuwa unakwenda na hatimaye Balozi Sefue akasema Timu yake ya uchunguzi imebaini Muhongo,Maswi hawana hatia Katika Escrow.

Zitto,Kafulila na wazushi wenzenu mmeumbuka, nendeni mkajipange upya ili mje na jungu jingine tena Kama mnafikiri mnaweza kuaminiwa tena Kuzusha majungu maana  mmeishajulikana Kuwa Nyie ni wataalamu wa kuwazusha baadhi ya mambo ambayo yanaleta taharuki Katika taifa na mwisho wa siku vyombo Vya upelelezi vikifanya uchunguzi tuhuma hizo inabainika ni uongo.

Na mfano  mzuri kipindi kile  Zitto alipozusha Kuwa anayoorodha ya Majina ya vigogo walioficha mabilioni nchini Uswiss   lakini Zitto alipotakiwa   na aliyekuwa  Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Fredrick Werema ambaye akilazimika kujiuzulu wadhifa wake kwa uzushi wenu  wa Escrow ulishindwa kutoa ushahidi huo wa majina hayo.

Zitto na Kafulila ,Filikunjombe katika ulingo wa siasa na hasa katika sakata la Escrow .  Mlikikuja na Spidi  ya moshi wa treni sasa    zimekwisha    zimebaki Kama vile  moshi wa sigala (fegi).Mtasubiri.

Hivi sasa mmekuwa  kama Midori. Mbele hamchezi ,nyuma hamtikisiki. Aibu yenu.

Mungu Ibariki Tanzania.

Facebook: Happy Katabazi
Mei 10 Mwaka 2015.




No comments:

Powered by Blogger.