Header Ads

LUSINDE 'AICHANA' UKAWA BUNGENI LEO


" NI kweli serikali ya CCM imechoka kwasababu imefanyakazi kubwa sana ya kujenga barabara,mahospitali,madaraja,kuleta maendeleo kwa taifa.

Hata gari likitembea umbali mrefu linachoka linaitaji kufanyiwa sevisi halafu linaendelea na safari. 

Kwani hata gari la Mwenyekiti wa Chadema,Freeman Mbowe na Tundu Lissu magari yakitembea umbali mrefu yakichoka  hawayatupi wanachokifanya ni kuyafanyia sevisi kisha magari hayo yanaendelea na safari.

Ndio maana nakiri CCM imechoka kwasababu imefanyakazi nzito ya kuleta maendeleo katika nchi ni lazima ichoke ipumzike halafu ndio maana kwenye kampeni za Oktoba mwaka 2015 ,CCM itaomba tena ridhaa ya wananchi ili irudi kuendelea kufanyakazi kubwa zaidi.

UKAWA hawajachoka kwasababu haijafanyakazi ngumu ,UKAWA imekuwa ikifanyakazi nyepesi sana na kazi hiyo ina herufi sita tu ambayo ni kusimama na kusema neno hili(HAPANA). Sasa mtu ambaye ana kazi moja tu ya kusema neno HAPANA kama UKAWA na Chadema ni wazi hawawezi kuchoka maana hawajafanya kazi nzito.Kusema HAPANA kwa kila kitu siyo kazi nzito ndiyo maana UKAWA hawajachoka.

UKAWA wamekuwa wakisema CCM imechoka kwasababu imekaa muda mrefu madarakani, mimi na waambia hivi Chadema wakati mwingine wanajitukana wenyewe kwasababu Mzee Mtei , Dk.Wilbroad Slaa ni wazee lakini ndiyo wanaiongoza Chadema na UKAWA ndio wanamtegemea Slaa awe mgombea urais wakati Slaa ni mgombea urais mzee kuliko wagombea wote na amechoka.

Jamani  Ikulu sio wodi ya wagonjwa,Ikulu watu wanatakiwa kwenda kufanyakazi sio kulazwa.

Nasema sumu haionjwi , Ukawa ni sumu na watanzania sio wajinga hawapo tayari kuona sumu kwa kuiweka UKAWA madarakani kwanza UKAWA una sera gani  na ni chama kilichosajiliwa wapi na nani?

Maana hili Chama kichaguliwe lazima kiuze sera zake kwa wananchi,wananchi waulizeni Ilani na sera za UKAWA ni zipi maana hakuna chama kilichosajiliwa kinaitwa UKAWA?

CCM ukawa wasitutishe ,hawana wameishakwisha mapema na ninawaakikishia UKAWA mtashindwa vibaya katika uchaguzi mkuu Oktoba mwaka huu.

Eti Mbunge wa Iringa Mjini (Peter Msigwa), anasema CCM ya CCM ni hatari kwa usalama wa Taifa  kwasababu Hazina hailipi madeni ya makandarasi na serikali ina madeni makubwa sana .

Kwanza amenishangaza sana huyu Msigwa,anajifanya kushangaa madeni inayodaiwa serikali lakini anashindwa kujishangaa kwanza yeye binafsi maana na yeye ana madeni alikopa hapa bungeni.

Mbona hashangai madeni tunayodaiwa sisi wabunge humu ndani maana kuna wabunge humu ndani tulikopa mikopo zaidi ya Sh.Milioni 200".

Maneno hayo ni miongoni mwa maneno yaliyozungumzwa na Mbunge wa Jimbo la Mtera (CCM), Livingstone Lusinde wakati akichangia hoja zake katika Bajeti ya ofisi ya Waziri Mkuu ,leo saa sita mchana,Mei 13 mwaka 2015.

Nampenda sana Lusinde kwa ubunifu wake wa maneno na kupambana na mahasimu wa kisiasa wa chama chake cha CCM na kupigania maendeleo ya wananchi.

Mungu ampe maisha marefu na afya njema ana arudi tena bunge lijalo aendeleze kazi aliyoianza katika Jimbo la Mtera.

Imendaliwa na Happiness Katabazi, Mei 13  mwaka 2015.
0716 774494
Chanzo: www.katabazihappy.blogspot.com

No comments:

Powered by Blogger.