Header Ads

WAFANYABIASHARA ACHENI KUTUMIWA NA WANASIASA KUENDESHA MIGOMO YA KUFUNGA MADUKA




Na Happiness Katabazi
KWA zaidi ya miezi nane sasa baadhi ya wafanyabiashara wenye   maduka katika mikoa mbalimbali wamekuwa wakigoma kufungua maduka yao kwa madai mapya kila awamu wanayogoma.

Mgomo wa kwanza walivyogoma walidai kuwa mashine za EFDS wanauziwa kwa gharama kubwa na kwamba hawawezi kuzinunua,kodi ni kubwa.

Mara wafanyabiashara wakazusha mgomo mwingine ambao wakaja na madai mapya kuwa hawana elimu ya kutosha kuhusu matumizi ya mashine ua EFDS hivyo wanaitaji elimu.

Hivi sasa wameibuka tena kivingine katika mikoa tofauti eti wakitaka  Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara nchini, Johnson Minja  ambaye Machi 25 mwaka huu, Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma kwasababu alikiuka masharti ya dhamana aliyopewa ikiwemo ya kutowazuia wafanyabiashara kufunga maduka yao wakati kesi yake ikiendelea aachiliwe huru ndipo watafungua maduka yao.

Akitoa taarifa mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya Mkoa wa Dodoma, Rebecca Mbilu, Mwendesha mashtaka wa serikali Rose Shio amesema kuwa upelelezi dhidi ya kesi hiyo umeshakamilika na kuiomba mahakama kutengua dhamana ya mshtakiwa kutokana na kukiuka masharti ya dhamana aliyopewa.
Amesema kuwa pamoja na hilo Mwenyekiti huyo amekuwa akiendelea kufanya mikutano na wafanyabiashara kwa ajili ya kuwahamasisha wasiendelee kulipa kodi kwa kutumia mashine za kielektroniki za EFDS kitendo alichosema kuwa ni kukiuka masharti ya dhamana aliyopewa.

Hata hivyo wakili wa mshtakiwa, Godfrey Wasonga ameiambia mahakama kuwa tangu mteja wake apewe dhamana hajawahi kuitisha mikutano na wafanyabiashara kwani hata juzi hakuwa na mkutano bali wafanyabiashara waliokuja mjini Dodoma kusikiliza kesi ya mwenyekiti huyo, waliposikia kuwa yupo Dodoma walikwenda kumsalimia baada ya kupata taarifa kuwa yuko katika hoteli ya Image Hill.

Hata hivyo hakimu Mbilu alisema kuwa ameridhika na hoja za upande wa mashtaka na hivyo akatengua dhamana ya Minja na kumtaka kubaki rumande hadi April Mosi mwaka huu ambapo kesi yake itakuja kwaajili ya kutajwa.

Watanzania ikumbukwe kuwa Tanzania ni nchi iliyojiamliwa kuongozwa kwa Katiba na sheria.

Na Ibara ya 107A ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, nanukuu:

" 107A.-(1) Mamlaka ya utoaji haki katika Jamhuri ya Muungano
itakuwa mikononi mwa Idara ya Mahakama na Idara ya
Mahakama ya Zanzibar, na kwa hiyo hakuna chombo cha Serikali
wala cha Bunge au Baraza la Wawakilishi la Zanzibar
kitakachokuwa na kauli ya mwisho katika utoaji haki.
 (2) Katika kutoa uamuzi wa mashauri ya madai na jinai kwa
kuzingatia sheria, Mahakama zitafuata kanuni zifuatazo, yaani:
(a) kutenda haki kwa wote bila ya kujali hali ya mtu kijamii Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzaniaau kiuchumi;
(b) kutochelewesha haki bila sababu ya kimsingi;
(c) kutoa fidia ipasayo kwa watu wanaoathirika kutokana
na makosa ya watu wengine, na kwa mujibu wa sheria
mahususi iliyotungwa na Bunge;
(d) kukuza na kuendeleza usuluhishi baina ya wahusika na katika migogoro; na
(e) kutenda haki bila kufungwa kupita kiasi na masharti ya kiufundi yanayoweza kukwamisha haki kutendeka.

Minja amefunguliwa kesi hiyo ya jinai na kwa makusudi ameamua kukiuka masharti ya dhamana upande wa jamhuri ukawasilisha ombi la kuomba afutiwe dhamana kwababu amekiuka masharti na mahakama ikakubaliana na ombi hilo kwasababu ina mamlaka ya kufanha hivyo.

Sasa haya madai ya kiuwendawazimu yaani yanayotolewa na  baadhi ya wafanyabiashara ambao wamedai wameamua kuanzisha mgomo wa kutofungua maduka eti  kushinikiza Mwenyekiti wao Minja aachiriwe uhuru hayo mamlaka ya kiuwendawazimu lazima watakuwa wameyapata kwa wendawazimu wenzao ambao ni baadhi ya  wanasiasa wanaowatumia wafanyabiashara hao wa maduka kufanya vitendo vya uwendawazimu vya kugoma kufungua maduka yao.

Nimelazimika kuwaita hawa wafanyabiashara wanaogoma wanafanya vitendo vya kiuwendawazimu na kweli kitendo chao hicho cha kugoma kufungua maduka kwasababu wanataka Minja aachiriwe huru ni cha kiuwendawazimu.

Kwababu mtu mwenye akili timamu ,anateheshimu sheria za nchi na anayejitambua,mwenye uchungu na taifa lake na asiyekubali kutumiwa na wanasiasa uchwara kama wanavyotumika hawa wafanyabiashara uchwara wanaogopa kufungua maduka yao kwa kutumia njia za kiuni hawezi kufanya hivyo.

Wasomi wa sheria wanamsemo mmoja usemao ' Haki yako inapoishia ndiyo haki ya mwenzako inapoanzia'.

Yaani kwa  maana ya msemo huo hapo juu kuwa wafanyabiashara wana haki ya kupata maslahi na wananchi wanaotaji kupata huduma kutoka kwa wafanyabiashara matokeo yake hawapati haki hiyo na serikali haipati haki yake ya kupata mapato.

Sasa hawa wafanyabiashara uchwara ambao minawaita wafanyabiashara ucharwa na wanaotumiwa na wanasiasa kwa lengo moja la kuakikikisha serikali inashindwa kupata mapato kwasababu ya mgomo huo na matokeo yake serikali itajikuta inakosa fedha za kuendesha mahospitali,huduma za kijamii muhimu kwasababu itakuwa haina fedha na mwisho wake wananchi kuichukia serikali yao na kuanza kuingia barabarani kufanya vurugu kushinikiza serikali itoke madarakani kwasababu imeshindwa kuwapatia  huduma muhimu.

Na mpango huo ndiyo ulioratibiwa na baadhi ya wanaisasa  hapa nchini kwa siri kwa kuwatumia hao wafanyabiashara uchwara ambao wengi wa wafanyabiashara wanatokea Mkoa mmoja wa Mikoa ya Kanda ya Kaskazini kufanya migomo hiyo kwa njia dhalimu.

Hata kama wafanyabiashara hao wana madai ya msingi lakini ni wazi baadhi ya wafanyabiashara hao wanatumia njia ambazo hazikubariki kisheria kudai haki zao.

Haya basi tufanye ni kweli mashine hizo hawawezi kuzinunua kwasababu bei yake ipo juu, wamepandishiwa kiwango kikubwa cha kodi na hawawezi kukimudu.

Nawauliza wafanyabiashara hawa hivi Mahakamani au kwenye Baraza la Rufaa la Kodi hawapajui?

Maana huko ndiko sehemu sahihi kwao kwenda kulalamikia hayo mambo mawili wanayoyapinga matokeo yake hawajaenda kulalamika huko wameishia kulalamika kwenye vyombo vya habari,serikalini na kwa hao mabwana zao wanasiasa wanaowatumia vibaya.

Ibara ya 13(6)(a) ya   Katiba ya nchi ,ninanukuu;

'Wakati haki na wajibu wa mtu yeyote vinahitaji
kufanyiwa uamuzi wa mahakama au chombo
kinginecho kinachohusika, basi mtu huyo atakuwa na
haki ya kupewa fursa ya kusikilizwa kwa ukamilifu, na
pia haki ya kukata rufaa au kupata nafuu nyingine ya
kisheria kutokana na maamuzi ya mahakama au
chombo hicho kingenecho kinachohusika'.

Kwa lugha nyepesi ibara hiyo nyie wafanyabiashara uchwara ibara hiyo  inatoa haki ya kukata rufaa katika mahakama ya juu kupinga uamuzi uliotolewa na mahakama ya chini kama unaona una sababu na haki (Locus of stand) ya kukata rufaa katika Mahakama ya juu.

Kwahiyo  nyie wafanyabiashara uchwara hamna haki ya kukata rufaa kupinga uamuzi wa mahakama wa kumfutia dhamana Minja ,mwenye mamlaka hayo ni  Minja mwenyewe na siyo nyie wafanyabiashara wala wanasiasa uchwara waliopayuka ndani ya bunge akiwemo Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi kutaka Minja apewe dhamana nje ya mahakama na siku zote mahakama inafanyakazi ndano ya mahakama siyo maneno ya kihuni uhuni yanayotolewa na wahuni huni nje ya mahakama kutaka apewe dhamana.

Na mtambue uhuni wenu huo wa shinikizo la kutaka Minja apatiwe dhamana,nyie siyo watu wa kwanza uufanya, aliiufanya Mwenyekiti wa Chama Cha CUF, Professa Ibrahim Lipumba wakati Sheikh Ponda Issa Ponda alipokamatwa Agosti mwaka 2012 na kufunguliwa kesi ya uchochezi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na Mkurugenzi wa Mashitaka nchini alimfungia dhamana kwa mujibu wa kifungu cha 148 (5) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2002 na Ponda kweli alikaa gerezani hadi  Mei 8 mwama 2013 alipofungwa kifungo cha mwaka mmoja nje.

Na siyo Lipumba peke yake bali baadhi ya waislamu wenzake nao walikuwa wakikesha misikitini na mahakamani kushinikiza aachiwe lakini wapi.

Sasa Minja ninani hadi na yeye mahakama ipindishe sheria ili impendelee?

Hivi Minja na Ponda nani mwenye nguvu ya watu na mwenye wafuasi wengi na akiamua kufanya jambo lake vyombo vya dola vinakesha macho kumsaka kama siyo Ponda lakini serikali imemdhibiti?

Mbinu yenu hiyo ya kijinga ndiyo itasababaisha Minja aendelee kusota gerezani.

Ndio maana minashawishika kuwafananisha nyie wafanyabiashara mliogoma hivi sasa kwa sababu eti mnataka Minja aachiriwe huru kwa  sawa  na wendawazimu kwababu zifuatazo:

Mosi , hamna haki ya kisheria nyie wafanyabiashara mambumbu wa sheria wa kuilazimisha mahakama ifanye mnavyotaka nyie.

Pili, mnaingilia majukumu ya kimahakama  ya kusikiliza na kutolea maamuzi kesi.

Tatu, nyie wafanyabiashara uchwara mliogoma hamna haki ya kwenda kukata rufaa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma kupinga uamuzi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma wa kumfutia dhamana  Minja kwasababu nyie siyo washitakiwa katika kesi hiyo.

Sasa kihelehele hiki cha kusema Minja kaonewa wakati hata usikilizwaji wa awali wa kesi hiyo haujafanyika  kinatoka wapi kama siyo ushambenga na ukosefu wa akili na kuipaka matope mhimili wa mahakama na kuleta fujo katika jamii yetu?

Watanzania wangapi wanafutiwa dhamana na  Mahakama mbona hamjawahi kuwa na umoja kiasi hiki na kufunga maduka?

Kwanini Minja tu? Kwa hiyo ikitokea mahakama isitengue amri yake ya kumfutia dhamana hadi mwakani ,nyie wafanyabiashara uchwara mtaendelea hadi mwakani na mgomo wenu  wa kutofungua madukani yenu hadi atakapopatiwa dhamai hapo mwakani?

Hivi zile leseni za biashara mlizopewa na serikali kwaajili ya nyie kuendesha biashara kuna mahali kokote zimeandikwa siku Mwenyekiti wa umoja wa wafanyabiashara akifutiwa dhamana basi ni ruksa kwa wafanyabiashara kugoma kufungua maduka?

Hivi hizo leseni za biashara zenu kuna sehemu yoyote  inaonyesha wafanyabiashara wataruhusiwa kisheria kugoma kufungua maduka yao kwasababu ya kupinga gharama za manunuzi ya mashine ya EFDS? Jibu ni hakuna.

Nawauliza nyie wafanyabiashara uchwara haya mamlaka  ya nyie baadhi ya wafanyabiashara ya kukaidi kununua mashine hiyo, kushiriki migomo isiyofuata taratibu za kisheria mmeyapata wapi na kwa mujibu wa sheria zipi hali inayosababisha wananchi kukosa huduma na kulipa kodi kwa serikali yao na serikali kushindwa kupata mapato?

Halafu tujiulize ni kwanini wafanyabiashara wenye asili ya Kiarabu na Wahindi hawagomi na wote wapo pale pale Kariakoo kwa hapa jiji la Dar es Salaam?

Na ni kwanini kila kukicha mfano Dar es Salaam, wanagoma wafanyabiashara wenye maduka eneo la Kariakoo tu?

Mbona wafanyabiashara wenye maduka yenye bidhaa zilizokidhi viwango kupita bidhaa zinazoouzwa katika maduka ya wafanyabiashara wagomaji katika maeno ya Posta Mpya, Sinza,Manzese, Mbezi ,Masaki na Kimara mbona hajuwasikia wakigoma na kufunga ofisi zao?

Kila kukicha ni wafanyabiashara wa Kariakoo.Kwanini? Maduka mengi ya Kariakoo inadaiwa yanamilikiwa  na watu wenye asili ya Kabila la Wachaga na Wakinga.

Iweje baadhi ya wafanyabiashara hawa wagomaji wadai hawana feha za kununulia mashine ya EFDS lakini wafanyabiashara hawa hawa wanamitaji inayowapa fursa ya wenda nchini Uturuki, China ,Kenya na Dubai kwenda kuchukua  mzigo  na kuuleta Tanzania na kisha kuuza?

Kwanza badhi ya wafanyabiashara wenye maduka hapo Kariakoo mnatuuzia bidhaa mbazo hazina ubora .

Lakini upole Watanzania ndio unawaa kiburi nyie wafanyabiashara kufanya uhuni we huu lakini mtambue kila jambo lina  mwisho wake.

Na uchunguzi wangu nilioufanya kabla sijaandika makala hii unaonyesha kuna baadhi ya wafanyabiashara wapo tayari kufungua maduka yao ila wanaogopa kushughulikiwa na wafanyabiashara wenzao ambao wanaendesha mgomo huo kwa maelekezo ya baadhi ya wanaisasa toka baadhi ya vyama ya upinzani hapa nchini.

Licha pia kuna baadhi ya wafanyabiashara wengine hapo Kariakoo wamefunga mlango wa mbele wa duka hilo anakaa mbele ya hilo duka na endapo anahisi anayepita mbele yake ni mteja anamuuliza kama anaitaji huduma na mteja yule akikubali, muuzaji wa duka hilo anampitishia mlango wa nyuma mteja yule na kisha anaenda kumpatia huduma bila kumpatia risiti hali inayosababisha serikali kuendelea kukosa mapato kutokana na uhuni huu unaofanywa na wahuni hawa yaani wafanyabiashara.

Ebu tujiulize mfanyabiashara wa ukweli na  mweye akili timamu na tujuavyo sisi wafanyabiashara wengi wanamikopo ya kuendeshea biashara zao na wanadaiwa kodi za pango, anakubalije kugoma kufanyabiashara na asiingize fedha  kwa sababu dhaifu kama hizo?

Nalazimika kuanza kukubaliana na Mwanasayansi ambaye ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Bagamoyo(UB) Dk.Elifuraha Mtaro ambaye kila siku anasema mitafaruku inayoendelea kuibuka kila kukicha ni Jiopolitiko Agenda, akiwa anamaanisha mtafuruku inayobuka kila kukicha ni ajenda chafu za baadi ya mataifa ya kigeni yasiyotaikia mema Tanzania, wanataka kuakiikisha siku watanzania tunachinjana  amani yetu inatoweka.

Uenda hawa wanaoendesha mgomo wa kutofungua maduka tayari wameishapatiwa fedha za uhakika na wabaya wa taifa hili ndio maana hata wasipoyafungua maduka yao hawana hasara kwasababu tayari walishapeww fedha za kutosha toka kwa  kwa mabwana zao wanaowatuma waanzishe migomo hiyo kila kukicha.

 Maana aingii akilini mfanyaboashara anayeendesha biashara ya duka lake kwa mkopo ,anatakiwa kila  baada ya muda fulani akarudishe  marejesho, anadaiwa kodi ya pango akubali kushiriki mgomo wa kugoma kufungua duka lake.

Maana Tanzania hivi sasa kila kukicha inaibuka mitafaruku ya kutikisa nchi na kuacha  makovu hali inayosababisha nchi hii hivi sasa ya kuibua na mitafaruku na siyo furaha tena.

Serikali nayo katika mgogoro huu wa wafanyabiashafa ,haiwezi kukwepa lawama hii kwamba imekuwa ikichelewa sana kuchukua maamuzi ya maana ambayo yangesebabisha hawa wafanyabiashara kurudia kugoma goma.

Nimekuwa nikijiuliza maswali bila majibu kwamba ni kwanini serikali inabembelezana sana na wafanyabiashara hawa ambao tangu mwanzo wanavunja sheria za nchi na kusababisha wananchi kukosa huduma na serikali kushindwa kupata mapato?

Je ni kwasababu baadhi ya viongozi wa serikali nao wanamgongano wa kimaslahi yaani wanatajwa wao binafsi ,familia zao kumiliki maduka katika maeneo hayo kama Kariakoo?

Maana aiingii akilini serikali yoyote ambayo kamwe haipotayari kuona inakoseshwa kupata mapato yake na wahuni wachache yaani hawa wafanyabiashara halafu iendelee kuwakumbatia  na kuwa kenulia meno.

Hawa wafanyabiashara wamekuwa na jeuri  kila wanapojisikia wanagoma  kwasababu uenda  wanadhani  serikali hii ni 'mhuni' mwenzao haiwezi kuwafanya chochote na ndio maana hata jana tumeshuudia madereva wa daladala kule  mjini Songea Mkoani Ruvuma nao waligoma utoa huduma kwa madai kuwa wanaunga mkono mgomo wa wafanyabaishara na wanashinikiza Minja aachiliwe huru.

Huu  mi nasema ni wazimu unaofanywa  na hao wenye madaladala na wafanyabiashara kwani kadri siku zinavyozidi kusoga mbele ndiyo mnavyodhiirisha huu siyo mgomo wa wafanyabiashara bali wafanyabiashara hao na madereva hao wa madaladala wanatekeleza kwa vitendo maelekezo ya wanasiasa uchwara ambao mara kwa  mara wamekuwa wakijiapiza nchi haitatawalika na kuiosesha mapato serikali.

Watu wenye akili timamu na wachunguzi wa  mambo tumelibaini hili.

Nawashauri wafanyabiashara mnaogoma  acheni kugoma rudini mfanyekazi na kama kweli mnafiriki mnamadai ya msingi basi fuateni njia utaratibu wa kisheria na kiungwana kudai madai yenu na siyo njia hii ya kihuni na kidhalimu mnayofanya.

Hao wanasiasa  wanaowatumia minawafananishaga na  Maibilisi kwani nyie siyo watu wa kwanza kuwatumiwa kutekeleza ajenda zao chafu  ambazo mwisho siku mtaumia nyie siyo wao.

Kawaulizeni baadhi ya wanafunzi wa Vyuo Vikuu, Madaktari,wakazi wa Mtwara kuzuia bomba la gesi lisijengwe, baadhi ya  wahitimu wa JKT .

Wanasiasa hao wenye tabia za kishetani waliyatumia makundi kikamilifu na mwisho wa siku makundi hayo ndiyo yaliyoathirika wale vinara wa JKT wapo gerezani, yule kinara wa mgomo wa madaktari kilichomkuta sote tunakifahamu nakilichowakuta wale baadhi ya wakazi wa Mtwara waliokuwa wakileta vurugu kuhusu bomba la gesi lisijengwe kilichowafika sote tunakifahamu na sio wanaisasa hao.

Bila shaka na nyie wafanyabiashara   mnawashwa mno mnaitaji mmpatiwe dawa ili muache kujikuna huo upelele unaowawasha hadi unasababaisha mnavunja sheria za nchi kwa makusudi na mtapatiwa dawa na wenye uchungu na nchi hii kama msipoacha huo uhuni wenu wa kuikosesha  mapato serikali na kutusabishia wananchi tukose huduma.

Sasa na nyie wafanyabiashara mnachokitafuta mtakipata kwasababu ushahidi uliopo wazi mmevuka mipaka sasa na mna ajenda  chafu nyuma pazi ya mgomo wenu siyo  mashine ya EFDS na huo ndiyo
 ukweli mchungu fungueni maduka mfanyebiashara kama biashara imewawashinda fungeni maduka ingieni kwenye ulingo wa siasa tuwajue kuliko kucheza na uchumi wa taifa letu kwa sababu za kipuuzi tu.

Kama kweli Tanzania ni taifa linalotaka kupiga  hatua za kimaendeleo kweli ,minashauri nyie wanasiasa uchwara wetu acheni tabia zenu chafu za kuingiza siasa zenu chafu katika masuala ya uchumi,mnaangamiza taifa kiuchumi kwa akili zenu mbovu na tamaa zenu za madaraka kwa kuuingiza siasa chafu katika mambo nyeti kama masuala ya uchumi,amani na usalama wa taifa letu.

Na serikali iache tabia ya kulealea ushetani huu kwa kuacha madhara yasambae ndiyo iibuke usingizini ijifanye inaanza kuchukua hatua.Ina kera sana.

Mungu ibariki Tanzania

Chanzo: Facebook: Happy Katabazi
Blogg: www.katabazihappy.blogspot.com
0716 774494
Aprili Mosi Mwaka 2015.

No comments:

Powered by Blogger.