Header Ads

MAHABUSU CHE MUNDUGWAO AFARIKI DUNIA








*TUJIKUMBUSHE KESI YAKE ILIVYOANZA

Na Happiness Katabazi

KWA wapenzi wa muziki wa asili  na watayarishaji wa vipindi va Redio Leo tume pokea kwa masikitiko taarifa za mwanamuziki  wa muziki wa asili nchini, Chingwale Che Mundugwao  (48) ambaye alikuwa akiishi gerezani kwasababu alikuwa akikabiliwa na Kesi ya wizi wa Passpot mali ya serikali tangu Aliposhitakiwa rasmi Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam,Juni 2 Mwaka 2013 na wenzake.

Makosa waliyokuwa wakishitakiwa nayo yaliyokuwa na dhamana kwa mujibu wa Sheria licha Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), kwa mamlaka aliyonayo kwa mujibu wa Kifungu cha 148(4) cha Sheria ya Mwendendo wa Makosa ya Jinai ya Mwaka 2002 , kinampa mamlaka kumfungia dhamana mshitakiwa yoyote anayekabiliwa na kesi ambayo Mashitaka yanayomkabili yanadhamana pindi atakupoona kunasa babu zenye maslahi ya taifa.

Kwahiyo tangu Juni 2Mwaka 2013, Che Mundugwao alikuwa Ni mahabusu na alikuwa  akiishi Katika Gereza la Keko . 

Na wakati akiishi gerezani Che Mundugwao alifiwa  na Mtoto wake lakini hakuweza kushiriki msiba wa mwanae Huyo kwasababu alikuwa gerezani chini ya Ulinzi , hivyo Che Mundugwao ,Leo amemfuata mwanae mavumbini.Huzuni.

Binafsi Che Mundugwao nilianza kumfahamu tangu Kipindi kile akiwa mwanamuziki wa muziki wa asili na Aliwahi kupiga Wimbo wake mmoja uliompatia  Umaarufu unaitwa 'TUMETOKA KWETU MAHENGE....TUMEKUJA  DAR ES SALAM KUJA KUCHEZA SINDIMBA '. Mwaka 2000.

Wimbo huu ulitamba Katika Miaka ya katikati ya miaka 1990 na Katika Wimbo huu miongoni mwa wanamuziki waliocheza Katika Wimbo huo ni Luiza Mbutu ambaye ni kiongozi wa Bendi ya Twanga Pepeta hivi sasa na dansi machachari wa Enzi hizo za Mwakambaye ambaye ni Mkazi wa Ubungo NHC, Lucas Mapunda 'Kimavi' ambaye alisoma shule ya Msingi Ubungo NHC , Dar es Salaam, na wakati huo Mimi nikisoma shule ya Msingi Mugabe na Tution nilikuwa nikisoma shule ya Msingi Ubungo NHC, hivyo tulikuwa tukikutana Mara kwa Mara Che Mundugwao Na Lucas Mapunda

Kwa mtakaoenda kutaza video ya Wimbo hiyo mtakubaliana na Mimi Kuwa  Luiza Mbutu ametoka mbali katika fani ya muziki na amebadilika sana.

Aidha Che Mundugwao aliendesha Kipindi cha Muziki wa Asili  Katika Redio Tumaini na hatimaye mwisho wa siku Juni 3 Mwaka 2013, Mimi nilipokuwa Mwandishi wa Habari  za Mahakamani wa Gazeti la Tanzania Daima, nilishuhudia Che Mundugwao aniletwa Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu siku hiyo kwa Mara ya kwanza mchana, akiwa chini ya Ulinzi wa Askari kanzu na kupandishwa kizimbani na kushitakiwa kwa Kesi iliyokuwa ikimkabili.

Nilisikitika sana  kuona Che Mundugwao kuwa mikononi mwa dola ila nilikuwa sina jinsi ya kumsaidia kwasababu licha alikuwa ni rafiki yangu, lakini Sheria ni Msumeno inakata kote kote na Mimi Kama Mwandishi wa Habari za mahakamani na waandishi wenzangu licha tulikuwa tukimfahamu Che Mundugwao ,bila woga tulikuwa tukitimiza jukumu letu la ku hatarisha umma ikiwa ni pamoja kwa kuripoti Kesi mbalimbali ikiwemo Kesi ya Che Mundugwao.
Mungu aiweke roho ya marehemu mahali panapostahili.Amina.


NOVEMBA 14 MWAKA 2013

UPELELEZI  KESI YA CHE MUNGUGWAO WAKAMILIKA

Na Happiness Katabazi

NOVEMBA  14 Mwaka 2013 upande wa jamhuri Katika Kesi hii ulieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ,Dar es Salaam, Kuwa upelelezi wa Kesi hiyo umekamilika.


JULAI  18 MWAKA 2013

KESI YA CHE MUNDUGWAO YAZIDI KUSOMBA WATU

Na Happiness Katabazi

WAKAZI wawili wa Dar es Salaam,jana walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu  kwaajili  ya hapo baadae kuja kuunganishwa katika kesi ya wizi wa Paspoti 26 inayomkabili Msainii wa Muziki wa asili, Chingwele Che Mundugwao na wenzake wanne.

Wakili wa serikali  Aidah Kisumo mbele Hakimu Mkazi Sundi Fimbo aliwataja washitakiwa hao walifikishwa jana kwa mara ya kwanza mahakamani hapo wakikabiliwa na makosa yanayofanana ambayo yanamkabili Chemundugwao na wenzake ni  Rajab Momba na Haji Mshamu.

JULAI 24 mwaka 2013 

WANNE WAONGEZWA KESI YA CHE MUNDUGWAO

Na Happiness Katabazi
 WAHUDUMU  wa wawili wa Idara ya Uhamiaji jana walifikishwa kalifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, nakuunganishwa katika kesi ya wizi wa Paspoti 26 inayomkabili Mwanamuziki wa muziki wa Asili nchini, Chingwele Che Mundugwao na wenzake  ambapo hadi kufikia jana kesi hiyo imefanya kuwa na jumla ya washitakiwa tisa akiwemo raia mmoja wa Uingereza.

Wakili wa Serikali Lasdsalaus Komanya mbele ya Hakimu Mkazi Sundi Fimbo 
alidai kuwa kesi hiyo jana ilikuja kwaajili ya kujatwa lakini,pia upande wa jamhuri imekusudia kufanya mabadiliko ya hati ya mashitaka ambapo jana imeweza kuwaunganisha washitakiwa wawili wapya ambao ni wahudumu wa Idara ya uhamiaji Adam Athuman na Abdallah Salehe  na washitakiwa wengine wawili ambao walifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Julai 18 mwaka huu ambao ni  Rajab Momba na Haji Mshamu katika kesi hiyo ya Che Mundugwao ambao inawashitakiwa watano na hivyo kufanya sasa kuwa na jumla ya washitakiwa tisa.

Washitakiwa wengine ni Che Mundugwao, Raia wa Uingereza Ahsan Iqbal au Ali Patel, Ofisa  Ugavi wa  Idara ya Uhamiaji Shemweta Kiluwasha, Injinia Keneth Pius wa Kikosi  cha Zimamoto na Uokoaji na mfanyabiashara Ally Jabir.

Hata hivyo washitakiwa hao walikanusha mashitaka hayo na kudai kuwa upelelezi bado haujakamilika na hivyo hakimu Fimbo aliarisha kesi hiyo hadi Agosti 5 mwaka huu, itakapokuja kwaajili ya kutajwa na akaamuru washitakiwa hao warejeshwe rumande kwasababu bado Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP), Dk.Eliezer Feleshi hajaondoa hati yake ya kuwafungia dhamana mahakamani.


Akiwasomea mashitaka wakili Komanya alidai kuwa tarehe isiyofahamika washitakiwa walikula njama ya kutenda kosa. Aidha tarehe tofauti Dar es Salaam, Momba aliiba hati ya kusafiria yenye namba AB 651926 mali ya serikali.

Alidai washitakiwa hao wa nne na wanadaiwa tarehe isiyofahamika Dar es Salaam, walighushi hati ya kusafiria yenye namba hiyo, kuonesha ni halali na imetolewa na Idara ya Uhamiaji ya Tanzania jambo ambalo si kweli.


JUNI 2 Mwaka 2013 

CHE MUNDUGWAO KORTINI KWA WIZI WA PASPOTI 26

*DPP AWAFUNGIA DHAMANA

Na Happiness Katabazi

MSANII wa muziki nchini, Chigwele Che Mundugwao 46, ofisa Manunuzi  wa Idara ya Uhamiaji, Shemweta Kilwasha (31), Mhandisi wa Idara ya Zimamoto na Ukoaji, Keneth Pius 37 na mfanyabiashara, Ally  Jabir ( 34) jana walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, wakikabiliwa na jumla ya mashitaka manne likiwemo kosa la wizi wa jumla ya Pasipoti 26.

Wakili Mwandamizi wa Serikali, Ladslaus Komanya  mbele ya Hakimu Mkazi  Aloyce Katemana wanakabiliwa na kosa la kula njama kutenda kosa hilo kinyume na kifungu cha  384 cha Sheria ya Kanuni ya adhabu ya mwaka 2002.
Wakili Komanya alieleza kuwa kati ya Aprili 16 na Mei 10, mwaka huu , Shimweta akiwa ni mtumishi wa umma,  katika Makao Makuu ya Idara ya Uhamiaji aliiba paspoti 26, mali ya Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Komanya alidai kuwa washitakiwa  Chigwele, Keneth na Ally, Mei 30, mwaka huu, huko Yombo Makangarawe jijini Dar es Salaam ,walikamatwa wakiwa na pasipoti hizo 26 za wizi.

Kuhusu  Che Mundugwao,wakili Komanya alidai kuwa mshitakiwa huyo kuwa Aprili 22, mwaka huu alikamatwa akimiliki  paspoti 12  za watu wengine bila ya kuwa na sababu yoyote ya msingi .

Wakili huyo wa Serikali, aliendelea kudai kuwa Mei , mwaka huu  Che Mundugwao pia alikamatwa na maofisa wanausalama akimiliki pasipoti nyingine mbili  zenye majina ya watu wengine sababu yoyote ya msingi. 
Komanya aliendelea kuwa Aprili 24 mwaka huu, mshitakiwa Ally , alighushi paspoti yenye namba AB 65196 akionyesha kuwa ilikuwa ni halali na kwamba ilitolewa na Idara ya Uhamiaji wakati akijua kuwa si kweli.

Wakili Komanya alidai kuwa kati ya mwaka 2007 na 2011 Dar es Salaam,   Shemweta alighushi nyaraka ya serikali ambayo ni muhuri akijaribu kuonyesha kuwa nyaraka hizo zilikuwa ni halali na kwamba zimetolewa na Idara ya Uhamiaji wakati si kweli.

Baada ya washtakiwa kusomewa mashtaka hayo, walikana na upande wa jamhuri ukadai  kuwa upelelezi bado haujakamilika.

Wakili Komanya alidai kuwa kutokana na asili ya makosa hayo, Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP),Dk.Eliezer Feleshi aliwasilisha hati ya kuzuia dhamana chini ya kifungu cha 148 (4) cha sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2002 na ataiondoa hati hiyo pale atakapoona hipo sababu ya kufanya hivyo ila kwasasa amefunga dhamana ya washitakiwa hao. 

Kiongozi wa jopo  la mawakili wanaowatetea washtakiwa hao, Peter Kibatala aliiomba mahakama kuwapa dhamana washtakiwa hao kwa sababu mashtaka yao yanadhaminika na kwamba hayapo katika vifungu ambayo vinazuia dhamana.

Hata hivyo Hakimu Katemana  aliiahirisha kesi hiyo hadi Juni 5, mwaka huu kwa ajili ya kutoa uamuzi juu ya hoja hizo zilizowasilishwa mahakamani hapo na akaamuru washitakiwa wote wapelekwe gerezani na kwamba Mahakama yake haina mamlaka ya kutoa dhamana kwasababu Kifungu hicho kilichotumiwa na DPP kimeifunga mkono mahakama kutoa dhamana kwa washitakiwa.

 Chanzo: www.katabazihappy.blogspot.com
Facebook: Happy Katabazi
0716 774494
Aprili 16 Mwaka 2015.


No comments:

Powered by Blogger.