Header Ads

KORTI YAAMURU MATANDIKO WA MSD ALETWE MAHAKAMANI



KORTI YAAMURU MATANDIKO WA MSD ALETWE MAHAKAMA
Na Happiness Katabazi
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, imeamuru mshitakiwa wa kwanza ambaye alikuwa ni Mkuuu Mkurugenzi  wa Operesheni Kanda ya Kaskazini wa Bohari Kuu ya Madawa(MSD),  Slyvester Matandiko  katika kesi ya matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia serikali hasara ya sh bilioni tatu aletewe mahakamani au hospitalini ili asomewe mashitaka yanayomkabili.

Amri hiyo ilitolewa Jana na Hakimu Mkazi Hellen Liwa  ambaye Alisema amekuba liana na ombi la Wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(PCCB), Leornad Swai  ambalo lilikuwa Linaomba Mahakama hiyo itoe amri ya upande wa jamhuri uende kumsomea Mashitaka Matindiko kwasababu tangu Kesi inayowakabiliwa jumla ya washitakiwa wa tano , mapema mwaka huu, ni washitakiwa wanne tu ndiyo waliosomewa mashitaka na mshitakiwa mmoja (Matandiko) bado hajasomewa mashitaka kwakile kinachdaiwa na upande wa utetezi Kuwa mshitakiwa Huyo ni mgonjwa na hawezi kufika mahakamani.


Ombi hilo liliwasilishwa jana na Mwendesha Mashitaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Leonard Swai, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Hellen Riwa.

Swai alidai kuwa washtakiwa wengine wameshasomewa mashitaka bila Matandiko kuwapo mahakamani kwa madai kuwa ni mgonjwa, hivyo kutokana na sababu hiyo, upande wa Jamhuri unaomba Mahakama kuhamia nyumbani kwa mshtakiwa huyo.

hakim Liwa Alisema anaiarisha Kesi hiyo hai Septemba 4 Mwaka huu itakapokuja kwaajili ya kutajwa  na kwamba Agosti 19 Mwaka huu, mshitakiwa Huyo asomewe Mashitaka.

Mbali na Matandiko ambaye ni Mkurugenzi wa Oparesheni Kanda ya Kaskazini wa MSD, wengine ni Naibu Mkurugenzi Mkuu wa MSD, ambaye pia ni Meneja wa Viwango, Sadiki Materu, Wasajili kutoka Bodi ya Maabara za Afya ni Zainabu Mfaume na Joseph Nchimbi.

Katika kesi ya msingi, washtakiwa wote kwa pamoja, wanakabiliwa na mashtaka saba, ya kutumia madaraka vibaya, na hivyo kuisababishia hasara serikali ya dola za Marekani 2,093,500, kwa kuruhusu uingizaji wa vitendanishi feki vya HIV nchini, na kuingizwa Bohari Kuu ya Dawa.
 
Wakati huo huo Kesi ya matumizi Mabaya a madaraka inayomkabili Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taneso, William Mhando imetajwa Jana na imearishwa hadi Agosti 26 Mwaka huu, Kwaajili ya kaunza kusikilizwa.

Chanzo: Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Agosti Mosi Mwaka 2014

No comments:

Powered by Blogger.