~ Kwa maoni yoyote kuhusu kazi zangu, niandikie katabazihappy@yahoo.com, au nipigie simu namba +255 755 312859. Asante kwa kunitembelea!~
Thursday, November 5, 2009
MAPYA YAIBUKA KESI YA MRAMBA,YONA
Na Happiness Katabazi

SHAHIDI wa pili katika kesi ya matumizi mabaya ya ofisi ya umma na kuisababishia serikali hasara ya sh bilioni 11.7, inayomkabili aliyekuwa Waziri wa Fedha, Basil Mramba na wenzake, Betha Msoka (44), ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kuwa hakuna mahali popote panapomlazimisha Waziri wa Fedha kuomba ushauri wa kutoa msamaha wa kodi Mamlaka ya Mapato nchini (TRA).

Sambamba na hilo, pia Msoka ambaye ni mwanasheria kitaaluma, amesisitiza kuwa hana ushahidi kwamba Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali haikushirikishwa kwenye mchakato wa kuitafuta Kampuni ya ukaguzi wa madini ya Alex Stewart Government Business Corporation.

Wakati shahidi huyo akitoa maelezo hayo, kwa mujibu wa hati ya mashitaka inasomeka kuwa washitakiwa hao wanakabiliwa na kosa la kukaidi ushauri wa TRA uliotaka kampuni hiyo isipewe msamaha wa kodi, lakini kwa nafasi zao waliamua kutoa msamaha huo.

Shahidi huyo wa upande wa mashitaka alitoa madai hayo jana mbele ya jopo la mahakimu wakazi; John Utamwa, Saul Kinemela na Sam Rumanyika wakati akihojiwa na mawakili wa utetezi; Hurbet Nyange, Peter Swai, Elias Msuya, Cuthbet Tenga na Profesa Shahidi.

Yafuatayo ni mahojiano baina ya mawakili hao na shahidi huyo:

Wakili: Ulishawahi kufanya kazi katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kama Mwanasheria wa Serikali?
Shahidi: Ndiyo.
Wakili: Ulifanya kazi katika ofisi hiyo kwa muda gani?
Shahidi: Sikumbuki ila nilifanya kazi kwa muda mfupi kwani nilipata barua toka Ofisi ya Utumishi ikiniarifu nahamishiwa Wizara ya Fedha.
Wakili: Hiyo barua ya Utumishi ilikuwa ni ya kukubadilisha kazi au kituo cha kazi?
Shahidi: Kituo cha kazi.
Wakili: Unayo hiyo barua inayokuonyesha umebadilishiwa kazi?
Shahidi: Sina.
Wakili: Tangu 1992 ulipohamishiwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, uliwahi kurudi katika ofisi hiyo kufanya kazi za ofisi hiyo?
Shahidi: Sikuwahi kurudi kwa sababu niliajiriwa na Wizara ya Fedha.
Wakili: Baada ya kutoka katika ofisi ya AG uliwahi kuwa na access ya majalada ya AG?
Shahidi: Sikuwahi kuwa na access ya kushika majalada ya ofisi hiyo.
Wakili: Je, nitakosea kama wewe ukiwa mtumishi wa serikali kama wakili wa serikali, ulikuwa ni daraja kati ya Wizara ya Fedha na ofisi ya AG?
Shahidi: Kuna masuala ambayo ofisi hizo mbili zilikuwa zikishirikiana.
Wakili: Nitakuwa sahihi nikisema masuala ya kisheria mnayoshirikiana na AG, ni Wizara ya Fedha ilikuwa inahusika moja kwa moja?
Shahidi: Mengi ni yale yaliyokuwa yanahusu Wizara ya Fedha moja kwa moja na mengine ambayo yana commontiment na wizara.
Wakili: Ulisema uliitwa BoT kujadili rasimu ya mkataba wa Alex Stewart, na ulibaini vipengele viwili vya kodi na ada, kipi kilikuwa kinahusu wizara yako?
Shahidi: Kipengele cha kodi kilikuwa kinahusu Wizara ya Fedha.
Wakili: Kipengele cha ada wewe akikukusumbua kama mwanasheria wa Wizara ya Fedha?
Shahidi: Ili msamaha wa kodi utolewe, ni lazima Waziri wa Fedha atoe idhini.
Wakili: Je, uliwasiliana na ofisi ya AG kuhusu hicho kipengele cha kodi?
Shahidi: Hatukuwasiliana na AG.
Wakili: Hivi Mramba, Yona na Mgonja wakati wakiwa na nyadhifa walikuwa ni wanasheria?
Shahidi: Hawakuwa na hadi sasa hawana taaluma ya sheria.

Wakili:Juzi uliieleza mahakama hii kwamba tangu uondoke ofisi ya AG ujawahi kurudi kufanyakazi hapo na nikakuuliza unasema uongo ,ukakataa.Kama unakumbuka dokezo la aliyekuwa Waziri wa Nishati(Yona)alilomwandikia Rais Benjamin Mkapa la Mei 11 mwaka 2003 linasomeka “Baada ya kukubali dokezo langu la Machi 3 mwaka 2003 kuhusu umuhimu wa kuanzisha ukaguzi wa dhahabu inayochimbwa na kuuzwa nchi za nje ,majadiliano kati ya Wizaya Nishati,Fedha,BoT na AG yanaenda vizuri’.Nikikwambia Wizara ya Nishati ilikuwa inawasiliana na na AG utasemaje?
Shahidi:Siwezi kujua.
Wakili:Kwahiyo wewe ulikwenda kwenye timu ya majadilio ya rasimu ya mkataba kama mwanasheria wa umma kwani sijakusikia wewe kama unataaluma ya uchumi?
Shahidi:Ndiyo nilikwenda kama mwanasheria.
Wakili:Wewe mwenyewe ulisema ulikuwa ni daraja kati ya Wizara ya Fedha na AG ,wewe uliona kuna haja katika timu hiyo kuletwa mwanasheria toka ofisi ya AG?
Shahidi:Watakuja watu wa ofisi ya AG watasema wenyewe.
Wakili:Una uhakika kama Wizara ya Nishati na Madini haikutafuta ushauri wa AG katika mchakato mzima wa kutafuta kampuni hiyo?
Shahidi:Sina uhakika.
Wakili;Jana ulisema uliandika barua TRA kuomba ushauri kuhusu kipengele cha msamaha wa kodi wa kampuni hiyo ,ebu ionyeshe mahakama hiyo barua?
Shahidi:Sina.
Wakili:Hiyo barua uliyoiandikia TRA kuhusu kipengele cha msamaha wa kodi , inamuweka Mramba kwenye nafasi nzuri.
Shahidi:Ndiyo inamuweka kwenye nafasi nzuri katika kutoa msamaha wa kodi.
Wakili: Una weza kujua ni kwanini upande wa mashitaka umeshindwa kukupa hiyo barua ili uitoe mahakamani kama kielelezo?
Shahidi:Sijui.
Wakili:Nikikwambia upande wa mashitaka umeiacha hiyo barua makusudi ili kumkandamiza mshitakiwa wa kwanza(Mramba)?
Shahidi:Sijui.
Wakili:Ulisema wizara ya Fedha inapotengeza matangazo ya serikali(government Notice) ni kwanini inashirikiana na ofisi ya AG?
Shahidi:Kwasababu matangazo hayo ya serikali ni nyaraka za kisheria.
Wakili:Je Gorvement Notice yakiakikiwa na AG halafu yakasainiwa na waziri wa Fedha, Je waziri akasini matangazo hayo ya serikali,kiongozi huyo anashtahili kulaumiwa?
Shahidi:Hastahili kulaumiwa.
Wakili: Ulisema ofisi ya AG haikuwa na mwakilishi kwenye timu yenu?
Shahidi:Ndiyo.
Wakili:Je hukumaanisha mchakato mzima haukurikisha ofisi ya AG?
Shahidi:Sikumaanisha hivyo.
Wakili:Utakubaliana namimi kwamba mchakato mzima ulishirikisha ofisi ya AG?
Shahidi:Sina hakika na hilo.
Wakili:Una fahamu kuwa Mei 2 mwaka 2003,AG alijibu barua ya Yona aliyomwandikia Machi 3 mwaka 2003?
Shahidi:Sifahamu.
Wakili:Nikikwambia barua hiyo ya AG ipo unaweza kubisha kwani?
Shahidi:Siwezi kubisha.
Wakili:Unaweza kutoa ushahidi kwamba hakukuwepo mawasiliano kati ya Wizara ya Nishati na ofisi ya AG katika mchakato wa kutafuta kampuni hiyo ya ukaguzi wa madini?
Shahidi:Sina.
Wakili:Timu yenu ilikuwa inawajibika kwa nani?
Shahidi:Gavana(Marehemu Daud Ballali).
Wakili: Unafahamu mchakato mzima ulitakiwa kusimamiwa na BoT kwa niabaya ya serikali?
Shahidi:Siwezi kujua.
Wakili:Juzi ulisema Gavana alisaini mkataba mkataba wa serikali na kampuni hiyo, mwingine aliyesaini huo mkataba ni nani?
Shahidi:Katibu wa BoT, Bosco Kimela na huyu Edwin Frolence alisaini kwaniabaya kampuni hiyo na mkataba ulisainiwa Juni 14 mwaka 2003.
Wakili:Timu yenu ya majadiliano ndiyo ilipelekea mkataba huo kusainiwa?
Shahidi:Ndiyo.
Wakili:Timu yenu ilikuwa huru kufanyakazi na wala haikuingiliwa na mtu?
Shahidi:sikumbuki.
Wakili:Hawa washitakiwa walishawahi kuingilia timu yenu?
Shahidi:Sijawahi kuwashuhudia wakiingilia timu yetu.
Wakili:Mkataba uliosaini ni matokeo ya timu yenu, Je ndiyo ulioweka kipengele cha kodi?
Shahidi:Siyo kwasababu kipengele katika timu yetu tulikiwa kando na pia isingewezekana kwani waziri hakuwa ameishatoa msamaha wa kodi kwa kampuni hiyo.
Wakili:Timu yenu ndiyo iliyopitisha ada ya kampuni hiyo iwe asilimia 1.9 na mkaiweka kwenye ule mkataba?
Shahidi:Ndiyo tuliweka ada hiyo.
Wakili:Unafahamu Juni 4 mwaka 2003 timu yenu ilimjulisha Yona kwamba suala la ada limeishamalizika na barua hiyo iliandikwa na Gavana?
Shahidi:Hilo silifahamu.
Wakili:Nikikwambia barua hiyo ipo?
Shahidi:Sibishi.
Waliki:Ulisema waziri ndiye mwenye mamlaka ya mwisho ya kutoa msamaha wa kodi sasa kwanini wewe ulipeleka barua TRA kuomba ushauri?
Shahidi:Ieleweke hakuna mahala popote panapomlazimisha waziri wa Fedha aombe ushauri wa msamaha wa kodi kwa kampuni yoyote kwa TRA.
Wakili:Mkataba huo ulikuwa unasemaje?
Shahidi:Ulisema Alex Stewart itasamehewa kodi zote.
Wakili:Jukumu la Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwenye matangazo ya serikali nini?
Shahidi:Ni kuakikisha matangazo ya serikali linakubalika kisheria.

Kesi hiyo iliahirishwa hadi Desemba 15-18 mwaka huu, itakapokuja kwa ajili ya shahidi wa tatu wa upande wa mashitaka kuanza kutoa ushahidi wake.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Novemba 6,2009



 
© Happiness Katabazi |Tarehe: 9:16 PM | Permalink | Maoni 0
MTALAAMU:NILISHAURI YONA KUACHANA NA ALEX STEWART
Na Happiness Katabazi

SHAHIDI wa kwanza katika kesi ya matumuzi mabaya ya ofisi ya umma, inayomkabili aliyekuwa Waziri wa Fedha, Basil Mramba na wenzake, Godwin Nyero (48), ameendelea kuiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam kuwa, waziri akiona ushauri uliotolewa na mtaalamu haufahi, anaweza kuukataa.


Nyero ambaye alikuwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Sheria na Masuala ya Uchumi katika Wizara ya Nishati na Madini, alitoa maelezo hayo jana mbele ya jopo la mahakimu wakazi; John Utamwa, Saul Kinemela na Sam Rumanyika wakati akijibu maswali aliyokuwa akihojiwa na Wakili Cuthbet Tenga na E. Msuya ambao wanamtetea mshitakiwa wa pili, Daniel Yona na Profesa Leonard Shahidi, anayemtetea mshitakiwa wa tatu, Gray Mgonja.

Shahidi huyo ambaye pia alikuwa mjumbe wa kamati ya kuandaa mchakato wa kuileta kampuni ya ukaguzi wa madini nchini ya Alex Stewart Government Business Corporation, alidai kuwa baada ya kumalizika kwa mchakato huo, alimpelekea dokezo aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Yona kutaka serikali isiipe kazi kampuni hiyo.

Hata hivyo, mawakili hao wa mshitakiwa wa pili walilazimika kuiomba mahakama isitishe kuendelea kumhoji shahidi huyo kutokana na upande wa mashitaka kushindwa kuleta nyaraka za mkataba wa serikali na kampuni hiyo ambazo walidai zingeletwa mahakamani hapo ili zitumike kumuuliza maswali.

Ombi hilo lilikubaliwa na jopo hilo ambalo liliuamuru upande wa mashitaka ulete nyaraka hizo Novemba 16 mwaka huu ili shahidi huyo aendelee kuhojiwa na mawakili hao.
Mahojiano kati ya shahidi huyo na mawakili hao yalikuwa hivi:

Wakili: Kwanini mapendekezo yako ya kuikataa kampuni hiyo hukutoa nakala kwa Katibu Mkuu na Kamishna wa Madini?
Shahidi: Katibu Mkuu nilimpatia taarifa kwa mdomo na Kamishna wa Madini sikumpatia taarifa.
Wakili: Ieleze mahakama mantiki ya kumpa waziri taarifa kwa maandishi, kamishna wa madini usimpatie taarifa na katibu mkuu umpatie kwa mdomo.
Shahidi: Mh! Ni taarifa tu ambayo nilimpa ushauri waziri (Yona) autumie yeye kama ataona unafaa na akiona haufahi pia kiongozi huyo wa wizara alazimiki kuniambia mimi mtaalamu.
Wakili: Waziri akiona ushauri wako wewe mtaalamu haufahi anakuwa amekosea?
Shahidi: Hajakosea.
Wakili: Kamishna wa Madini kama ulimwambia ushauri huo kwa mdomo alikujibu nini?
Shahidi: Alinijibu nimwandikie dokezo waziri wangu.
Wakili: Ni kweli kwamba kulikuwa na ulazima wa serikali kuleta mkaguzi wa dhahabu hapa nchini kufuatia malalamiko ya wabunge na wananchi kwamba madini yetu yanaibwa?
Shahidi: Ni kweli.
Wakili: Malalamiko ya wabunge yalijitokeza bungeni?
Shahidi: Ndiyo.
Wakili: Serikali ilivyoanza mchakato wa kuipata kampuni hiyo ilikuwa inatekeleza matakwa ya Bunge?
Shahidi: Hilo sifahamu.
Wakili: Kamati yenu ya watu wanne iliteuliwa rasmi lini?
Shahidi: Sikumbuki.
Wakili: Yawezekana ilikuwa Septemba 12, 2002?
Shahidi: Yawezekana.
Wakili: Mwenyekiti wa kamati yenu alikuwa nani?
Shahidi: Sikumbuki.
Wakili: Katibu Mkuu wa kamati hiyo alikuwa nani?
Shahidi: Sikumbuki ila najua wajumbe wenzangu watatu walitoka BoT.
Wakili: Hao wajumbe watatu walikuwa wataalamu wa mambo gani kwenye hiyo kamati yenu kwa sababu wewe ulishaiambia mahakama ulikuwa mtaalamu wa madini?
Shahidi: Sifahamu.
Wakili: Kabla ya kwenda kwenye hiyo kamati mlipewa mwongozo wa kufanya kazi?
Shahidi: Sikumbuki.
Wakili: Mlikuwa mnatumia utaratibu gani wa kufikia uamuzi?
Shahidi: Consensus.
Wakili: Ni kweli kwamba na wewe ulikuwa unafikia consensus hiyo?
Shahidi: Ndiyo.
Wakili: Consensus inafikiwa baada ya majadiliano ya wajumbe wanne?
Shahidi: Ndiyo.
Wakili: Juzi uliiambia mahakama kwamba masuala yenye utata mliyapeleka kwa gavana na yasiyo na utata kwenye kamati yenu yaliendelea kujadiliwa?
Shahidi: Ndiyo.
Wakili: Hiyo kamati yenu ilifanya kazi yake kwa uhuru bila kuingiliwa na washitakiwa waliopo kizimbani?
Shahidi: Ndiyo.
Wakili: Kwanini ulipeleka mambo msiyokubaliana kwa Waziri Yona badala ya Gavana?
Shahidi: Kwa maelekezo ya waziri alivyonituma kazi, nikitoka kwenye kamati hiyo niwe namletea taarifa.
Aidha, shahidi wa pili, Betha Msoka (44), ambaye ni mwanasheria kitaaluma na kati ya mwaka 1992-2003 alikuwa ni ofisa mwandamizi msimamizi wa fedha toka Wizara ya Fedha, aliiambia mahakama kuwa mwaka 2003 alipewa maelekezo na mkuu wake kitengo cha huduma ya sheria wizarani hapo, Agness Bukuku ambaye sasa ni Msajili wa Hazina, akaiwakilishe wizara katika majadiliano ya mkataba wa kampuni hiyo ya ukaguzi wa madini na wizara yake.
Soka alidai aliudhuria majadiliano hayo yaliyoshirikisha wataalamu toka wizara ya Fedha,Nishati na Benki Kuu na majadiliano yalihusu mkataba wa mkaguzi wa madini ya dhahabu katika ya serikali ya Tanzania na Alex Stewart Gorvement Corporation ya Marekani na kwamba vikao vilijadili rasimu ya mkataba huo na baada ya kupitia walibaini vipengele vingi vya kitaalamu vinavyohusu Kodi na Ada.

Yafuatayo ni mahojiano kati ya Shahidi huyo na Wakili Mkuu wa Serikali Stanslaus Boniface:
Wakili:Hayo mambo mawili yalishughulikiwa vipi katika majadiliano yenu?
Shahidi:Suala la Ada lilishughulikiwa na Wizara ya Nishati.Na mkataba huo kwangu ulikuwa ni mgeni kwangu kwasababumimi nilikuwa natokea Wizara ya Fedha ,nilitizama kipengele cha kodi kwa makini.
Wakili:Baada ya kutizama kwamikini vipengele hivyo vilisema nini?
Shahidi:Vilikuwa vinatoa msamaha wa kodi kwa kampuni hiyo na wataalamu wake.
Wakili:Wewe ulishughulikia vipi jambo hilo?
Shahidi:Mimi niliwaeleza wajumbe wenzake kwamba mwenye mamlaka ya mwisho ya kusamehe kodi ni Waziri wa Fedha kwahiyo hadi tupate ridhaa toka kwa waziri.
Wakili:Baada ya kuwaeleza hilo, wenzio majibu yao yalikuwaje?
Shahidi:Ni kitu ambacho waliamua kukiweka kando hadi Waziri atoe idhini.
Wakili:Wewe kama mwakilishi wa wizara ya Fedha ulifanyanini?
Shahidi:Nilimjulisha mkuu wangu wa kazi(Agnes Bukuku) kwa njia ya maandishi na baada ya kumueleza alikubaliana nami na barua ikaandikwa kwenda TRA kwaajili ya kuhusu vipengele vile viwili yaani vya ada na kodi.
Wakili:Namna gani ulishughulikana na kampuni hiyo ya ukaguzi?
Shahidi:Sikushiriki majadiliano tangu siku barua ya ushauri ilipopelekwa TRA wala sikujua nini kiliendelea kwani sikuitwa tena kwenye kikao.
Wakili:TRA walijibuje hiyo barua?
Shahidi:Ilisema kampuni hiyo haistahili kusamehewa kodi.
Wakili:Katika Timu yenu ya majadiliano ya mkataba huo alikuwepo mwakilishi toka ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali?
Shahidi:Hakuwepo.
Wakili:Soma hiki kielelezo cha kwanza, katika aya ya tano inasomekaje?.
Shahidi:Kielelezo hiki ni dokezo la Yona alilomwandikia Rais Mkapa,Machi 3 mwaka 2003,kinasomeka: ‘Kabla ya BoT haijachagua kampuni inayofaha itazingatia mapato ya serikali yasipungue na wawekezaji wasiumie kiasi cha kukata tama kuwekeza zaidi kwenye madini .Aidha tutapa ushauri toka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Wakili:Soma tena na kielelezo hiki cha tatu kinasomekaje?
Shahidi:Hiki ni barua aliyoiandika Yona kwenda kwa rais Mkapa Mei 11,2003 na kinasomeka hivi: ‘Baada ya kukaandikia dokezo langu Machi 3 mwaka 2003 kuhusu umuhimu wa kuanzisha ukaguzi wa dhahabu inayochimba na kuuzwa nchi za nje , majadiliano kati ya Wizara ya Nishati.Fedha,BoT na Mwanasheria Mkuu wa Serikali yanaendelea vizuri.

Kesi hiyo inayovuta hisia za wengi, inaendelea tena ambapo mawakili wa utetezi wataanza kumhoji shahidi huyo wa pili.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi Novemba 5,2009
 
© Happiness Katabazi |Tarehe: 8:41 PM | Permalink | Maoni 0
Wednesday, November 4, 2009
KESI YA MRAMBA,YONA YAIBUA MAPYA
Na Happiness Katabazi

SHAHIDI wa kwanza katika kesi ya matumuzi mabaya ya ofisi ya umma, inayomkabili aliyekuwa Waziri wa Fedha, Basil Mramba na wenzake, Godwin Nyero (48), ameendelea kuiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam kuwa, waziri akiona ushauri uliotolewa na mtaalamu haufahi, anaweza kuukataa.


Nyero ambaye alikuwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Sheria na Masuala ya Uchumi katika Wizara ya Nishati na Madini, alitoa maelezo hayo jana mbele ya jopo la mahakimu wakazi; John Utamwa, Saul Kinemela na Sam Rumanyika wakati akijibu maswali aliyokuwa akihojiwa na Wakili Cuthbet Tenga na E. Msuya ambao wanamtetea mshitakiwa wa pili, Daniel Yona na Profesa Leonard Shahidi, anayemtetea mshitakiwa wa tatu, Gray Mgonja.

Shahidi huyo ambaye pia alikuwa mjumbe wa kamati ya kuandaa mchakato wa kuileta kampuni ya ukaguzi wa madini nchini ya Alex Stewart Government Business Corporation, alidai kuwa baada ya kumalizika kwa mchakato huo, alimpelekea dokezo aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Yona kutaka serikali isiipe kazi kampuni hiyo.

Hata hivyo, mawakili hao wa mshitakiwa wa pili walilazimika kuiomba mahakama isitishe kuendelea kumhoji shahidi huyo kutokana na upande wa mashitaka kushindwa kuleta nyaraka za mkataba wa serikali na kampuni hiyo ambazo walidai zingeletwa mahakamani hapo ili zitumike kumuuliza maswali.

Ombi hilo lilikubaliwa na jopo hilo ambalo liliuamuru upande wa mashitaka ulete nyaraka hizo Novemba 16 mwaka huu ili shahidi huyo aendelee kuhojiwa na mawakili hao.
Mahojiano kati ya shahidi huyo na mawakili hao yalikuwa hivi:

Wakili: Kwanini mapendekezo yako ya kuikataa kampuni hiyo hukutoa nakala kwa Katibu Mkuu na Kamishna wa Madini?
Shahidi: Katibu Mkuu nilimpatia taarifa kwa mdomo na Kamishna wa Madini sikumpatia taarifa.
Wakili: Ieleze mahakama mantiki ya kumpa waziri taarifa kwa maandishi, kamishna wa madini usimpatie taarifa na katibu mkuu umpatie kwa mdomo.
Shahidi: Mh! Ni taarifa tu ambayo nilimpa ushauri waziri (Yona) autumie yeye kama ataona unafaa na akiona haufahi pia kiongozi huyo wa wizara alazimiki kuniambia mimi mtaalamu.
Wakili: Waziri akiona ushauri wako wewe mtaalamu haufahi anakuwa amekosea?
Shahidi: Hajakosea.
Wakili: Kamishna wa Madini kama ulimwambia ushauri huo kwa mdomo alikujibu nini?
Shahidi: Alinijibu nimwandikie dokezo waziri wangu.
Wakili: Ni kweli kwamba kulikuwa na ulazima wa serikali kuleta mkaguzi wa dhahabu hapa nchini kufuatia malalamiko ya wabunge na wananchi kwamba madini yetu yanaibwa?
Shahidi: Ni kweli.
Wakili: Malalamiko ya wabunge yalijitokeza bungeni?
Shahidi: Ndiyo.
Wakili: Serikali ilivyoanza mchakato wa kuipata kampuni hiyo ilikuwa inatekeleza matakwa ya Bunge?
Shahidi: Hilo sifahamu.
Wakili: Kamati yenu ya watu wanne iliteuliwa rasmi lini?
Shahidi: Sikumbuki.
Wakili: Yawezekana ilikuwa Septemba 12, 2002?
Shahidi: Yawezekana.
Wakili: Mwenyekiti wa kamati yenu alikuwa nani?
Shahidi: Sikumbuki.
Wakili: Katibu Mkuu wa kamati hiyo alikuwa nani?
Shahidi: Sikumbuki ila najua wajumbe wenzangu watatu walitoka BoT.
Wakili: Hao wajumbe watatu walikuwa wataalamu wa mambo gani kwenye hiyo kamati yenu kwa sababu wewe ulishaiambia mahakama ulikuwa mtaalamu wa madini?
Shahidi: Sifahamu.
Wakili: Kabla ya kwenda kwenye hiyo kamati mlipewa mwongozo wa kufanya kazi?
Shahidi: Sikumbuki.
Wakili: Mlikuwa mnatumia utaratibu gani wa kufikia uamuzi?
Shahidi: Consensus.
Wakili: Ni kweli kwamba na wewe ulikuwa unafikia consensus hiyo?
Shahidi: Ndiyo.
Wakili: Consensus inafikiwa baada ya majadiliano ya wajumbe wanne?
Shahidi: Ndiyo.
Wakili: Juzi uliiambia mahakama kwamba masuala yenye utata mliyapeleka kwa gavana na yasiyo na utata kwenye kamati yenu yaliendelea kujadiliwa?
Shahidi: Ndiyo.
Wakili: Hiyo kamati yenu ilifanya kazi yake kwa uhuru bila kuingiliwa na washitakiwa waliopo kizimbani?
Shahidi: Ndiyo.
Wakili: Kwanini ulipeleka mambo msiyokubaliana kwa Waziri Yona badala ya Gavana?
Shahidi: Kwa maelekezo ya waziri alivyonituma kazi, nikitoka kwenye kamati hiyo niwe namletea taarifa.
Aidha, shahidi wa pili, Betha Msoka (44), ambaye ni mwanasheria kitaaluma na kati ya mwaka 1992-2003 alikuwa ni ofisa mwandamizi msimamizi wa fedha toka Wizara ya Fedha, aliiambia mahakama kuwa mwaka 2003 alipewa maelekezo na mkuu wake kitengo cha huduma ya sheria wizarani hapo, Agness Bukuku ambaye sasa ni Msajili wa Hazina, akaiwakilishe wizara katika majadiliano ya mkataba wa kampuni hiyo ya ukaguzi wa madini na wizara yake.
Soka alidai aliudhuria majadiliano hayo yaliyoshirikisha wataalamu toka wizara ya Fedha,Nishati na Benki Kuu na majadiliano yalihusu mkataba wa mkaguzi wa madini ya dhahabu katika ya serikali ya Tanzania na Alex Stewart Gorvement Corporation ya Marekani na kwamba vikao vilijadili rasimu ya mkataba huo na baada ya kupitia walibaini vipengele vingi vya kitaalamu vinavyohusu Kodi na Ada.

Yafuatayo ni mahojiano kati ya Shahidi huyo na Wakili Mkuu wa Serikali Stanslaus Boniface:
Wakili:Hayo mambo mawili yalishughulikiwa vipi katika majadiliano yenu?
Shahidi:Suala la Ada lilishughulikiwa na Wizara ya Nishati.Na mkataba huo kwangu ulikuwa ni mgeni kwangu kwasababumimi nilikuwa natokea Wizara ya Fedha ,nilitizama kipengele cha kodi kwa makini.
Wakili:Baada ya kutizama kwamikini vipengele hivyo vilisema nini?
Shahidi:Vilikuwa vinatoa msamaha wa kodi kwa kampuni hiyo na wataalamu wake.
Wakili:Wewe ulishughulikia vipi jambo hilo?
Shahidi:Mimi niliwaeleza wajumbe wenzake kwamba mwenye mamlaka ya mwisho ya kusamehe kodi ni Waziri wa Fedha kwahiyo hadi tupate ridhaa toka kwa waziri.
Wakili:Baada ya kuwaeleza hilo, wenzio majibu yao yalikuwaje?
Shahidi:Ni kitu ambacho waliamua kukiweka kando hadi Waziri atoe idhini.
Wakili:Wewe kama mwakilishi wa wizara ya Fedha ulifanyanini?
Shahidi:Nilimjulisha mkuu wangu wa kazi(Agnes Bukuku) kwa njia ya maandishi na baada ya kumueleza alikubaliana nami na barua ikaandikwa kwenda TRA kwaajili ya kuhusu vipengele vile viwili yaani vya ada na kodi.
Wakili:Namna gani ulishughulikana na kampuni hiyo ya ukaguzi?
Shahidi:Sikushiriki majadiliano tangu siku barua ya ushauri ilipopelekwa TRA wala sikujua nini kiliendelea kwani sikuitwa tena kwenye kikao.
Wakili:TRA walijibuje hiyo barua?
Shahidi:Ilisema kampuni hiyo haistahili kusamehewa kodi.
Wakili:Katika Timu yenu ya majadiliano ya mkataba huo alikuwepo mwakilishi toka ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali?
Shahidi:Hakuwepo.
Wakili:Soma hiki kielelezo cha kwanza, katika aya ya tano inasomekaje?.
Shahidi:Kielelezo hiki ni dokezo la Yona alilomwandikia Rais Mkapa,Machi 3 mwaka 2003,kinasomeka: ‘Kabla ya BoT haijachagua kampuni inayofaha itazingatia mapato ya serikali yasipungue na wawekezaji wasiumie kiasi cha kukata tama kuwekeza zaidi kwenye madini .Aidha tutapa ushauri toka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Wakili:Soma tena na kielelezo hiki cha tatu kinasomekaje?
Shahidi:Hiki ni barua aliyoiandika Yona kwenda kwa rais Mkapa Mei 11,2003 na kinasomeka hivi: ‘Baada ya kukaandikia dokezo langu Machi 3 mwaka 2003 kuhusu umuhimu wa kuanzisha ukaguzi wa dhahabu inayochimba na kuuzwa nchi za nje , majadiliano kati ya Wizara ya Nishati.Fedha,BoT na Mwanasheria Mkuu wa Serikali yanaendelea vizuri.

Kesi hiyo inayovuta hisia za wengi, inaendelea tena ambapo mawakili wa utetezi wataanza kumhoji shahidi huyo wa pili.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi Novemba 5,2009
 
© Happiness Katabazi |Tarehe: 8:09 PM | Permalink | Maoni 0
MKAPA ALIPULIWA MAHAKAMANI
.YADAIWA ALITOA IDHINI KULETWA ALEX STEWART
.SHAHIDI ADAI YONA ASINGEKATAA AGIZO LA RAIS
Na Happiness Katabazi

RAIS mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa anadaiwa kuandika barua iliyomtaka aliyekuwa Waziri wa NiShati na Madini, Daniel Yona kuharakisha mchakato wa kuileta Kampuni ya Alex Stewart Government Business Corporation kuja nchini kufanya ukaguzi wa dhahabu.


Yona ni mshitakiwa wa pili katika kesi ya matumizi mabaya ya ofisi na kuisababishia serikali hasara ya sh bilioni 11.7. Pamoja nae washitakiwa wengine ni aliyekuwa Waziri wa Fedha, Basil Mramba na aliyekuwa Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Gray Mgonja.

Kuhusika kwa Mkapa kulibainishwa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, na shahidi wa kwanza wa upande wa Jamhuri, Godwin Nyero (48) mbele ya jopo la mahakimu wakazi; John Utamwa, Saul Kinemela na Sam Rumanyika, wakati akihojiwa na wakili wa utetezi, Hurbet Nyange.

Nyero, aliyekuwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Sheria na Masuala ya Uchumi katika Wizara ya Nishati na Madini, alitoa maelezo hayo baada ya wakili Nyange kumtaka asome kwa sauti kielelezo namba 10 kilicholetwa mahakamani hapo na upande wa mashitaka, ambacho ni barua iliyotoka kwa Mkapa akimjibu Yona.

“Kwa mujibu wa barua ya Rais Mkapa aliyomjibu Yona, inasomeka kama ifuatavyo: Nakubaliana na ombi lako Waziri Yona na ninataka wizara yako iendelee na mchakato huo haraka,” ilisomeka sehemu ya barua hiyo.

Shahidi huyo, jana alionekana kuzungumza baadhi ya maelezo mapya yaliyokuwa yakitofautiana na aliyoyatoa juzi wakati akiongozwa na wakili wa mashitaka. Alidai kuwa licha ya yeye kumpatia mapendekezo yaliyokataza serikali isifanye haraka kuikubali Kampuni ya Alex Stewart kwa sababu haikuwa na mtaji wa kutosha, Yona asingeweza kukataa maagizo ya Rais Mkapa yaliyomtaka kuendelea na mchakato wa kuileta kampuni hiyo nchini.

Aidha, mahojiano kati ya shahidi huyo na wakili wa utetezi yalikuwa kama ifuatavyo:

Wakili: Juzi ulitamba hapa mahakamani kwamba wewe ulikuwa mtaalamu na ulitoa ushauri wako kwa Yona wa kuikataa hiyo kampuni, lakini mshitakiwa alipuuza. Je, ilikuwaje serikali ilikubali wewe ujiuzulu na isikatae ombi lako kwa gharama yoyote?

Shahidi: Sijui. Ninachofahamu mimi nilijiuzulu.

Wakili: Katika kamati yenu, wewe ulishauri nini kuhusu Alex Stewart?

Shahidi: Nilishauri isipewe tenda.

Wakili: Kuna andiko lolote uliloandika kwenye kamati hiyo kwamba hukubaliani na kampuni hiyo kupewa tenda?

Shahidi: Mh! Sina andiko la kuthibitisha hilo.

Wakili: Tutaamini vipi kama ushauri huo wa kitaalamu ndiyo huo huo ulimshauri Yona?

Shahidi: (Kimya)

Wakili: Sasa Yona alikosea nini kama si wewe ndiye uliyeisaliti kamati yako?

Shahidi: Hapana.

Wakili: Kwa hiyo unataka kusema walioisababishia serikali hasara ni wajumbe wenzako wa kamati?

Shahidi: Siwezi kusema hilo.

Wakili: Hii asilimia 1.9 ya malipo ya ada kwa kampuni hiyo, kamati yenu iliikubali?

Shahidi: Hatukuipitisha, tulifanya ulinganisho.

Wakili: Mlipitisha kampuni hiyo ilipwe ada asilimia ngapi?

Shahidi: Sikumbuki.

Wakili: Baada ya kamati yenu kuandaa ‘proposal’, kulifanyika tathimini ya kuipata kampuni hiyo, je, wewe ulishiriki kufanya tathimini kwa kampuni hizo mbili?

Shahidi: Nilishiriki.

Wakili: Tathimini ilionyesha Alex Stewart Government Business Corporation ilipata pointi ngapi?

Shahidi: Sikumbuki.

Wakili: Nakukumbusha, kampuni hizo mbili mlizipa alama za ushindi, Alex Stewart mliipa asilimia 92.9 na Walker & World mliipa asilimia 73.3.

Shahidi: Ni kweli.

Wakili: Ukiwa mtaalamu wa masuala ya madini, ni kampuni gani hapo ilikuwa na mafanikio zaidi ya kupata tenda?

Shahidi: Alex Stewart.

Wakili: Kamati ilipendekeza ni kampuni gani ipewe kazi ya kukagua dhahabu?

Shahidi: Alex Stewart.

Wakili: Wewe ulikuwepo kwenye kamati wakati pendekezo hilo linatolewa?

Shahidi: Ndiyo.

Wakili: Kwa mujibu wa kielelezo cha kumi, baada ya kamati yenu kutoa pendekezo hilo kwa serikali, wewe uliwazunguka wajumbe wa kamati yako na ukaenda peke yako kwa Yona na ukamwambia kampuni hiyo isipewe kazi, si ndiyo?

Shahidi: Ndiyo.

Wakili: Wewe unajua Yona ni mtu mmoja katika serikali hii, ni kwa nini ulifanya hivyo?

Shahidi: (Kimya)

Wakili: Huu mkataba wa serikali na kampuni hiyo si ulitokana na mapendekezo ya kamati yenu?

Shahidi: Sikumbuki.

Wakili: Ndiyo maana awali wakati naanza kukuhoji nilikwambia wewe wakati unafanya kazi Wizara ya Nishati na Madini ulikuwa hupikiki chungu kimoja na wenzio. Mwanzo uliiambia mahakama kamati yenu ilipendekeza kampuni ipewe kazi, sasa hivi unasema ilikataa isipewe kazi.

Shahidi: Kimya( wananchi wanaoudhuria kesi hiyo wakaangua vicheko).

Wakili: Kwa hiyo shahidi umeanza siyo kubadili maelezo yako kwamba kamati yenu ilipendekeza kampuni hiyo ipewe tenda?

Shahidi: Sikumbuki kamati kwamba tulipendekeza au tulisema imeshindwa kutimiza vigezo.

Wakili: Ni mapendekezo gani mlipeleka kwa Gavana marehemu Daud Balali kuhusu kampuni hiyo?

Shahidi: Mapendekezo kwamba Alex Stewart ilishinda.

Wakili: Baada ya kamati yenu kumpelekea mapendekezo hayo, mlitegemea gavana afanye nini?

Shahidi: Sijui (watu wakaangua vicheko)… Tulichotegemea aiite kampuni hiyo na aieleze imeshinda tathimini na wakubaliane namna ya kufanya kazi na makubaliano hayo yawekwe kwenye mkataba.

Wakili: Ndugu shahidi, ulishawahi kufanya utafiti wa madini katika nchi nyingine?

Shahidi: Hapana.

Wakili: Unajua hupaswi kuzungumzia kitu kama hujakifanyia utafiti, sasa ni kwanini unadai uliandika pendekezo kwa Yona kwamba tenda ya kampuni hiyo isitishwe na badala yake ufanyike utafiti katika nchi nyingine kwanza?

Shahidi: (Kimya)

Wakili: Kuna mahali popote wewe binafsi uliwahi kutoa taarifa kwa gavana kwamba hukubaliani na wajumbe wenzio?

Shahidi: Hapana.

Wakili: Mapendekezo yenu yaliyopelekwa kwa gavana uliwahi kuyaona?

Shahidi: Hapana.

Wakili: Wewe ulimshauri Waziri Yona kwamba hakuna haraka ya kuingia mkataba na kampuni hiyo. Nakuuliza akiambiwa na wakubwa wake aruhusu kampuni hiyo ije nchini kufanya kazi angekataa?

Shahidi: Hapana asingeweza kukataa.

Wakili: Nakwambia sasa Yona alimuandikia barua rais wa wakati huo Benjamin Mkapa akimuarifu kuhusu serikali kuitaka kampuni hiyo ije ifanye kazi ya ukaguzi hapa nchini na rais alimjibu barua hiyo ambayo naomba uisome kwa sauti.

Shahidi: Inasomeka kwamba. “Nakubaliana na taarifa yenu na endeleeni na mchakato wa kuipata kampuni hiyo haraka.”

Wakili: Sasa kama Rais Mkapa alimuagiza Yona aendelee na mchakato, waziri angeendelea kusikiliza ushauri wako wa kukataa serikali isitishe tenda na kampuni hiyo wakati wewe ni mdogo kimadaraka?

Shahidi: Ni kweli Yona asingeweza kukataa agizo la Mkapa.

Wakili: Uliwahi kuusoma ule mkataba?

Shahidi: Hapana, nilisoma rasimu ya mkataba na wala sikuona kipengele kilichonitatiza isipokuwa kipengele cha ada ya asilimia 1.9.

Wakili: Unavifahamu hivi vitabu?

Shahidi: Ndiyo, ni kumbukumbu ya majadiliano katika Bunge.

Wakili: Majadiliano ya Bunge mwaka 2004 uliyafuatilia?

Shahidi: (Kimya)

Wakili: Chukua hiki kitabu kimoja fungua ukurasa wa 25, kisha usome kwa sauti ili mahakama ijue unasema nini.

Shahidi: Unasomeka miswaada ya sheria ya nyongeza na matumizi ya fedha mwaka 2004.

Wakili: Kwa hiyo kuna uwezekano wa kufanyika ‘supplementary’ bajeti kabla ya mwaka wa fedha kuisha?

Shahidi: Ndiyo.

Wakili: Juzi uliiambia mahakama bajeti ya mwaka 2003/2004, haikutengwa bajeti ya malipo ya kampuni hiyo na kwamba Benki Kuu na wizara ilitumia njia zake kutafuta fedha kuilipa kampuni hiyo. Je, nikikwambia hii hansad inasema bajeti hiyo ilikuwa na nyongeza ya bajeti?

Shahidi: Ukisema hivyo ina maana hauna bajeti.

Wakili: Kwa hiyo ukipata nyongeza ya bajeti unakuwa hauna bajeti?

Shahidi: Unakuwa na bajeti.

Wakili: Zoezi la kuileta kampuni hiyo nchini lilikuwa halina faida yoyote?

Shahidi: Kifedha halina faida na kule kuthibitisha hakuna wizi wa madini yetu ni faida.

Wakili: Na nikikwambia sababu ya kampuni hiyo kushindwa kufanya kazi yao sawasawa ilitokana na kampuni za uchimbaji wa madini kukataa kukaguliwa?

Shahidi: Sijui.

Wakili: Unakumbuka aliyekuwa Waziri wa Fedha (Mramba) aliziita kampuni za uchimbaji wa madini nchini akazionya na kuzitaka zikubali kukaguliwa na kampuni hiyo?

Shahidi: Sawa kabisa Waziri wa Fedha alitenda hilo.

Wakili: Unakumbuka kampuni hiyo ilikataa taarifa za mahesabu za kampuni zinazochimba dhahabu hapa nchini zilizoonyesha zimepata hasara?

Shahidi: Hiyo sikumbuki.

Wakili: Unakumbuka sababu za serikali kuongeza mkataba na kampuni hiyo mwaka 2005 hadi 2007 ili iwezeshe kampuni hiyo kumaliza kazi yake ya ukaguzi iliyocheleweshwa na kampuni zilizokataa kukaguliwa?

Shahidi: Ni kweli.

Wakili: Kwa hiyo serikali iliingia hasara miaka miwili kwa sababu kampuni hizo zilikataa kukaguliwa, halafu wewe leo hii unatetea kampuni hizo hazijaitia hasara serikali?

Shahidi: Hiyo ni sababu mojawapo.

Wakili: Unajua nyaraka 6,000 zilifichwa na kampuni hizo za uchimbaji ili Kampuni ya Alex Stewart isizikague?

Shahidi: Ni zaidi ya 6,000.

Wakili: Hivi una habari hizo nyaraka zaidi ya 6,000 zilifichwa kwa ajili ya kukwepa kodi?

Shahidi: Hilo nalijua.

Wakili: Kama hilo unalijua asante sana kwani hizo nyaraka zilizofichwa ziligunduliwa na Kampuni ya Alex Stewart.

Shahidi: (Kimya)

Wakili: Unaifahamu Kampuni ya Plaser Dom na Resolut zilikuwa zinachimba madini, na katika ukaguzi Kampuni ya Alex Stewart iligundua zimeshindwa kuthibitisha matumizi ya dola 160 kwa sababu nyaraka zilikuwa Makao Makuu ya kampuni zao na si hapa nchini, nje ya nchi?

Shahidi: Hapana.

Wakili: Unajua nyaraka za kampuni za madini zinatakiwa zibaki hapa hapa nchini?

Shahidi: Najua.

Wakili: Wataalamu wenzio wametoa taarifa serikalini, wamesema takwimu za upatikanaji wa dhahabu ni za uongo, lakini wewe unasema takwimu za upatikanaji ni sahihi, tuamini lipi?

Shahidi: (Kimya)

Wakili: Hapa ninalo dokezo lililopokelewa na Spika wa Bunge kwamba Alex Stewart iligundua upungufu mkubwa katika uchimbaji na usafirishaji dhahabu, sasa unataka kusema kamati ilikosea?

Shahidi: Najua, ila siwezi kulisemea hilo.

Wakili: Juzi, uliiambia mahakama hii tukufu kwamba Alex Stewart haikutoa mafunzo kwa Watanzania?

Shahidi: Ni kweli ila kwa upande fulani.

Wakili: Una ushahidi wa hilo unalosema?

Shahidi: Sina hakika.

Wakili: Kama huna uhakika ni kwanini unadai kampuni hiyo haikutoa mafunzo kwa Watanzania?

Shahidi: (Kimya, watu wakaangua vicheko)

Wakili: Sasa tumepokea taarifa, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Arthur Mwakapugi, kupitia gazeti la The Citizen aliuambia umma kwamba hivi sasa Tanzania inatumia wataalamu Watanzania waliopata mafunzo ya ukaguzi wa madini toka Kampuni ya Alex Stewart. Je, utabisha?

Shahidi: Sibishi.

Hata hivyo, kiongozi wa jopo la mahakimu wakazi, Utamwa, aliahirisha kesi hiyo hadi leo na kumtaka shahidi huyo wa kwanza afike mahakamani ili endelee kuhojiwa na mawakili wa utetezi kwa kuwa jana kwa saa nne mfululizo alihojiwa na wakili Nyange, ambaye anamtetea Mramba.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Novemba 4,2009
 
© Happiness Katabazi |Tarehe: 7:42 PM | Permalink | Maoni 0
KESI YA MRAMBA YAANZA KUUNGURUMA
na Happiness Katabazi

SHAHIDI wa kwanza katika kesi ya matumizi mabaya ya ofisi ya umma na kuisababishia serikali hasara ya sh bilioni 11.7 inayomkabili aliyekuwa Waziri wa Fedha, Basil Mramba na wenzake wawili, Nyero Matihiza (48), ameieleza mahakama kuwa ushauri wake wa kitaalamu alioutoa ulipuuzwa na viongozi wake.


Mbali na Mramba washitakiwa wengine ni aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Daniel Yona na Katibu Mkuu Mstaafu Gray Mgonja.Wanaotetewa na mawakili wa kujitegemea Hurbet Nyange, Peter Swai, Profesa Leonard Shaidi, Cuthbert Tenga.

Matihiza ambaye alikuwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Sheria na Masuala ya Uchumi katika Wizara ya Nishati na Madini wakati huo ikiongozwa na mshitakiwa wa pili, Daniel Yona, alitoa madai hayo jana mbele ya jopo la mahakimu wakazi John Utamwa, Saul Kinemela na Sam Rumanyika wakati alipokuwa akiongozwa kutoa ushahidi wake na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Fredrick Manyanda na Stanslaus Boniface.

Matihiza alidai kitaalum yeye ni Diolojia alieleza yeye alikuwa mmoja wajumbe wa Kamati iliyopewa jukumu la kuaandaa mchakato wa kutafuta kampuni ya nje itakayokuja nchini kwaajili ya kukagua thamani na kiasi cha dhahabu kinachopatika kwasababu jamii ilikuwa ikitilia shaka takwimu ya dhahabu inayopatikana nchini haina ukweli wowote.

“Kamati yeti ilifanyakazi yake vyema na nilitoa mapendekezo kwa waziri wangu enzi hiyo(Yona)kwamba Kampuni ya Alex Stewart Gorvenment Bussiness Corporation imeshindwa kazi na ilikuwa imelenga kuficha ukweli na pia nikapendekeza kuwa ada ya asilimia 1.9 inayolipwa kampuni hiyo ni kubwa sana na zabuni itangazwe upya.”alidai Matihiza.

Ifuatayo ni mahojiano kati ya wakili wa serikali Manyanda na shahidi huyo.

Wakili:Wakati ukiwa na wadhifa huo, majukumu yako yaliyokuwa yapi?
Shahidi:Kuishauri wizara ya Nishati na Madini katika masuala ya sheria ya madini,uwekezaji katika sekta hiyo na mfumo wa kodi katika eneo hilo.
Wakili:Unajua nini kuhusu Mineral Assayers?
Shahidi:Ni ufuatiliaji wa madini yaliyo katika sampuli tofauti,mfano katika miamba dhahabu inapatikana kiasi gani.
Wakili:Unafahamu nini kuhusu Gold Asseyers Tanzania?
Shahidi: Mwaka 2002 nakumbuka kulikuwa na suala la wasiwasi kwa wananchi,wabunge kwamba makampuni yanayochimba madini yanaficha takwimu za ukweli kwahiyo kwahiyo majibu ya wakaguzi wa madini yalikuwa yakitiliwa wasiwasi.
Wakili:Kwanini kulikuwa na wasiwasi wa takwimu hizo?
Shahidi:Suala la uchimbaji wa madini katika taifa letu lilikuwa ni geni nandiyo maana wananchi walikuwa wanawasiwa kwamba madini yanayopatikana nimengi kuliko takwimu zonazotajwa.Na wizara iliamua kutafuta mkaguzi wa dhahabu ili kujua kitu gani kinaendelea kwenye sekta ya madini na baada ya hapo wizara kwa kushirikiana na BoT walipewa jukumu la kutafuta mkaguzi wa kutafiti dhahabu nchini.Wizara iliunda timu ya watu wanne na mimi nilikuwa mmoja wao ,tukafanyakazi yakuandaa maombi ya kutafuta mkaguzi wa dhahabu.
Wakili:Timu yenu ilitoa mapendekezo gani katika zoezi hilo la utafiti?
Shahidi:Tulipendekeza uwepo mifumo ya usimamizi ya uchimbaji wa madini,kukiaki taarifa za upatikanaji wa dhahabu na tukaweka vigezo kwamba kampuni ya ukaguzi wa madini tunayoitafuta isitokee kwenye nchi ambayo wachimbaji wa hapa nchini wametokea.
Wakili:Ni makampuni yapi mlipata baada ya kutangaza hiyo tenda?
Shahidi:Tulipata makampuni matano ambayo yalijitokeza ila ni kampuni moja ya Alex Stewart Asserys ndiyo ilishinda zabuni.
Wakili:Ni nani hao Alex Stewart Asseys?
Shahidi:Ni kampuni ambayo inafanya shughuli za ukaguzi wa madini Uingereza pia inatawi Marekani Na hiyo kampuni ya marekani ambayo ndiyo ilipewa kazi hapa nchini inaitwa Alex Stewart Government Bussiness Corporation.
Wakili:Alex Stewart Asseys na Alex Stewart Gorvement Bussiness Corporation zinahusiano gani?
Shahidi:Alex Stewart Asseys ni kampuni mama na hiyo nyingine ambayo inadaiwa inafanyakazi na serikali mbalimbali duniani na ndiyo maana serikali yetu ikaitafuta.Na ilitimiza vigezo vingi ila kigezo cha mtaji kilichomtaka alete vifaa(mahabara )hapa nchini kilimshinda na ndiyo maana kamati yetu tukaona hicho ni kikwazo kwetu.
Wakili:Mlifanya nini baadaya kuona haitimizi kigezo hicho?
Shahidi:Sisi kama kamati tulipeleka mapendekezo kwa Gavana marehemu Daudi Balali kwani nyiyo aliyekuwa anatusimamia.Na nimi nilipeleka dokezo kwa aliyekuwa waziri wa Nishati, Yona.
Wakili: Baada ya majadiliano yenu na kampuni hiyo nini kilifuata?
Shahidi:Uliandaliwa mkataba na ofisi ya Gavana.Waandaaji wa mkataba misikushiri ila nilishiriki kutoa mapendekezo.
Wakili;Mapendekezo ya kuikataa kampuni hiyo ya ukaguzi wa dhahabu uliandika lini?
Shahidi:Kabla ya mkataba kusainiwa na mapendekezo yangu niliyatoa wakati draft ya mkataba.
Wakili;Ni mapendekezo gani hayo?
Shahidi:Ada ya asilimia 1.9 kwa kampuni hiyo ilikuwa ni kubwa sana ikataliwe kwasababu taifa linapata mrahaba wa dhahabu wa asimilia 3.Hivyo nasisitiza mapendekezo yangu ya kitaalamu niliyompelekea Yona hakuzingatiwa.
Wakili:Utendaji wa Kampuni ulitakiwa uweje kwa mujibu wa mkataba?
Shahidi:Kuimarisha udhibiti na usimamizi na tulika kampuni hiyo itusaidie lakini haikuweza kutusaidia,eneo jingine ni ambalo utendaji wake haukulidhisha ni eneo la takwimu kwani katika mkataba kampuni hiyo iliaidi kupandisha takwimu za ukaguzi hadi asilimia 50 lakini ilishindwa kutimiza hilo,eneo jingine ni mafunzo kwa wataalum wa nchini ili kampuni hiyo ikimaliza muda wake na kuondoka wataalamu wetu waweze kuendelea.
Wakili:Bajeti ya 2003-2004 malipo ya mkaguzi huyo yalikuwemo?
Shahidi:Halikuwemo.

Kiongozi wa Jopo la mahakimu wakazi John Utamwa, aliairisha kesi hiyo hadi leo ambapo upande wa utetezi utakuja kumhoji shahidi huyo.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Novemba 3,2009
 
© Happiness Katabazi |Tarehe: 7:28 PM | Permalink | Maoni 0
MEREY BALHABOU AFUTIWA KESI
Na Happiness Katabazi

MFANYABIASHARA maarufu nchini, Merey Ally Saleh, maarufu kwa jina la Merey Balhabou na mwenzake, Abdallah Said Abdallah, waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya wizi wa dola milioni 1.08 (zaidi ya sh bilioni moja) , wamefutiwa mashitaka.


Washitakiwa hao wamefutiwa mashitaka baada ya Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP) kuwasilisha hati ya kuwafutia mashitaka washitakiwa hao katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Merey na mwenzake, wameachiwa huru chini ya kifungu 91(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, ambacho kinampa mamlaka DPP kuwaondolea mashitaka watuhumiwa.

Kuachiliwa kwa washitakiwa hao kunafanya washitakiwa katika kesi hiyo kwa njia ya mtandao wa kompyuta, mali ya Benki ya Barclays kubaki tisa.

Washitakiwa waliobaki katika kesi hiyo ni Winford Mwang’onda, Shubira Mutungi, Naima Saria, Upendo Mushi, Magreth Longway, Emmanuel Mukoni na Ramadhani Khamis, ambao ni wafanyakazi wa benki hiyo na mfanyabiashara, Justice Rugaibura.

Washitakiwa hao Oktoba 29-30 mwaka jana, walikula njama katika eneo lisilofahamika jijini Dar es Salaam, walifanya udanganyifu na kuiibia benki hiyo fedha hizo.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Novemba 3,2009
 
© Happiness Katabazi |Tarehe: 7:16 PM | Permalink | Maoni 0
Monday, November 2, 2009
TAKUKURU ISIWATISHE WABUNGE
Na Happiness Katabazi

BABA wa Taifa, hayati Julius Nyerere, aliwahi kusema kwamba ‘ukweli una tabia moja nzuri sana. Haujali mkubwa wala mdogo , haujali adui wala rafiki’.


Kuwahoji wabunge wakati Bunge linangojea kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa serikali kuhusu maazimio ya Kamati Teule yaliyotokana na uchunguzi wa kashfa ya kampuni ya kufua umeme ya Richmond ni ufisadi wa kupindukia.

Katika malumbano kati ya wabunge na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), taasisi hiyo imeungwa mkono na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kujaribu kuwahoji wabunge eti kuhusu sakata la kupokea posho mbilimbili.

Ukweli umeibuka kwamba zipo njama za kulizuia Bunge lisiwe na msimamo wa kuikataa taarifa itakayotolewa na serikali kuhusu utekelezaji wa maazimio ya Bunge kuhusu kashfa ya mkataba wa kampuni ya mfukoni ya Richmond.

Ni kweli kwamba katika ripoti aliyoiwasilisha aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge kuchunguza kashfa ya mkataba huyo, Dk. Harrison Mwakyembe, Februari mwaka jana, ilikubaliwa na kupitishwa na Bunge. Ndani ya ripoti hiyo liko pendekezo la kuwajibika kwa Mkuu wa Takukuru, Dk. Edward Hosea.

Mtu huyo (Dk.Hosea) sasa amechukua jukumu la kutaka kuwahoji wabunge hasa Dk.Mwakyembe.

Ni zuzu gani asiyekuwa na hata chembe ya uelewa wa sheria za nchi hata ashindwe kugundua kwamba Takukuru inatumia vibaya mamlaka yake kulitisha Bunge kwa jambo ambalo halina maslahi kwa taifa letu?

Kama wabunge watakubali vitisho hivyo vya kitoto na wakashindwa kujadili kikamilifu taarifa ya serikali kuhusu utekelezaji wa maazimio ya Bunge kuhusu Richmond, hapo itakapowasilishwa ili kuifurahisha Takukuru, hilo litakuwa ni janga la kitaifa na vita dhidi ya ufisadi vitakuwa vimeshindwa na mafisadi wanaweza kushangilia kwa nderemo na vifijo na kugonganisha glasi za mvinyo!

Sheria ya rushwa haina kipengele chochote kinachozuia takrima na wala wabunge kupokea posho mbili, hivyo kupokea posho mbili si kuvunja sheria za nchi ambazo tumeridhia zituongoze.

Kumhoji mtu kwenye jambo ambalo halijakatazwa kisheria ni kumtisha, kumfunga mdomo, kumkera na kumdhalilisha na pia ni upotevu wa rasilimali za taifa.

Labda Takukuru pekee ndiyo isiyojua kwamba muda watakaoutumia kuwahoji wabunge kwa jambo la ajabuajabu na kuchekesha, unalipiwa na walipakodi hivyo ni hasara kwa taifa?

Waziri Mkuu alipojiingiza katika jambo hili kwa kuruhusu mahojiano hayo baina ya wabunge na Takukuru yafanyike, hakuzingatia kwamba taasisi inayohusika inatuhumiwa mbele ya Bunge kwa hiyo kuiruhusu iwahoji wabunge ni kutojua sheria na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977.

Tunasema tumechoka sasa kwani ni miaka miwili serikali inasuasua na kujikanyagakanyaga kutekeleza maazimio ya Bunge! Kuna nini ndani yake?

Ikiwa kikao hiki cha Bunge kitashindwa kuiwajibisha serikali na kulimaliza suala hilo, basi ni wajibu wa sisi wananchi kuiadhibu serikali na wabunge wake katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.

Kwa upande wa Takukuru ni wazi kuwa sasa taasisi hii imepoteza heshima yake kwa kuparamia baadhi ya mambo bila kufanya utafiti wa kina.

Imekuwa ikipeleka baadhi ya kesi mahakamani bila ya kuwa na ushahidi wa kutosha na inazingatia zaidi majungu na mizengwe ya kisiasa kuliko maslahi ya taifa.

Yawezekana kwamba baadhi ya viongozi wakuu wa taasisi hiyo hivi sasa ni sehemu ya ufisadi na ni wala rushwa, makuwadi siasa za uporaji wa rasilimali za wananchi.

Ndiyo maana sintashangaa wavuja jasho kuiita taasisi hiyo taasisi ya kuhamasisha rushwa na siyo kuzuia.

Nimalizie kwa kuwaasa wabunge kwamba katu wasikubali kuhojiwa na Takukuru kwa sababu hakuna sheria ya nchi yoyote waliyoivunja, na ninawataka Takukuru na wale wote ambao wanakerwa na wabunge kupata posho mbilimbili, waone wakati umefika sasa wa kuibana serikali ili ipeleke muswada bungeni ambao utazuia wabunge na wafanyakazi wa taasisi nyingine iwe kwenye sekta binafsi na serikalini kupokea posho mbili.

Sasa kama hilo tukishindwa kulifanya, tutabaki kubwatabwata na kubwabwaja mitaani na kwenye vyombo vya habari.

Ieleweke itakuwa ni sawa na kumvalisha mbu miwani. Wabunge waliopokea na wanaoendelea kupokea posho mbili hawajavunja sheria za nchi na Takukuru inalijua hilo vizuri tu ila kwa sababu imeamua kutumia vibaya taasisi yetu hiyo kwa maslahi ya watu wachache inaamua kufanya kama ifanyavyo.

Takukuru inataka kuwahoji wabunge ili kuwahamisha fikra wananchi na wabunge kuacha kufuatilia hoja kuu ya ufisadi inayosababisha umaskini wa kutupwa kwa wavuja jasho.

Nataka Takukuru na Waziri Mkuu Pinda mfahamu kwamba sisi baadhi ya wananchi na waandishi wa habari wenye misimamo thabiti na upeo wa kuona mbali, tunaofahamu vyema kusoma alama za nyakati ‘hatudanganyiki’! Hii imekula kwenu na si kwa wavuja jasho!

Mungu ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika

0716 774494

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumapili, Novemba 1, 2009
 
© Happiness Katabazi |Tarehe: 3:58 PM | Permalink | Maoni 0